Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Kula Kondoo Aliyenona

kula kondoo aliye nona
Photo by Raul Ling on Pexels.com

Kama umeamua kula kondooo kula aliyenona haswaaa, Kiasi kwamba hutojutia kabisa hata kama alikuwa kondoo wa wizi

Ukiamua kutenda dhambi basi itende haswaaa maana hakuna dhambi ndogo

Mfano umeamua kuiba sasa kwanini unaiba kitu kidogo? Ikitokea umekamatwa yani upo tayar kuuliwa kisa kitu chenye thamani ndogo?? Kweli!?

Ukitaka kuwa mtakatifu basi jitakase haswaaa maana dini haina majaribu wala haitaki utani

Ukiamua kufanya Biashara ifanye haswaaa kwa uwezo wako wote kiasi kwamba hata kama ukishindwa usibaki na dukuduku na ukishinda usemee eeh yes kwa nguvu kubwa…

Kamwe kamwe usiwe mtu kati katika maisha yako

Kwamba hukai wala husimami, huendi wala haurudi kiufupi upo kama hujui nini unataka!

Simama eneo moja ujulikane na vaa uhusika uliouchagua wote hata kama unafanya jambo dogo zuri au baya

Fanya mpaka wengine wameze mate na watamani kuiga mfano wako hata kama nyuma walikupinga.

Jiamini na amini kwenye njia uliyoichagua kwa asilimia zote hata kama ni njia ndogo.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Jifunze Kushukuru

Next Post

Hakuna Marefu Yasiyo Na Ncha

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Usiogope Kujaribu

Usiogope kujaribu jambo hata kama unahisi huliwezi au ni gumu sana Kataa kabisa neno haiwezekani kwenye akili…