Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Wewe Ndio Dereva Wa Maisha Yako

wewe ndio dereva wa maisha yako
Photo by Markus Spiske on Pexels.com

Siku utakapojua kuwa watu wanaosema wanakupenda kwa sasa kuna siku watawaambia maneno hayahayo watu wengine Ndio siku utayojua kuwa unapaswa kuiamini nafsi yako pekee!

Siku utakayoelewa kuwa ikitokea umekufa waliokaribu yako wote watakusahau ndani ya muda mfupi na kuendelea na maisha yao Ndio siku utaacha kuishi kwa kutaka kumridhisha kila mtu

Endapo utaelewa kuwa kila anaeonesha kama anakufatilia na kukuchunguza kiuhalisia wala hana muda na wewe na anaumizwa na maisha yake binafsi Ndio ungegutuka na kuishi maisha yako bila kuogopa watu

Kama ungepata nafasi ya kuoneshwa siku utakayokufa basi uhakika ni kuwa kuna mambo mengi usingeyafanya hapa Duniani hasa kuumia kwa ajili ya vitu vinavyopita.

Maisha ni yako na wewe ndio dereva hivyo yaendeshe upendavyo.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Hakuna Marefu Yasiyo Na Ncha

Next Post

Tengeneza Bahati Yako Mwenyewe

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Tengeneza Mabawa Yako

Usikubali mazingira yakwamishe ndoto zako wala kukupa vikwazo vya kuwa unavyojiona kwa ndani Usikubali watu…