Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Usiogope Kujaribu

usiogope kujaribu
Photo by Nina Uhlikova on Pexels.com

Usiogope kujaribu jambo hata kama unahisi huliwezi au ni gumu sana

Kataa kabisa neno haiwezekani kwenye akili yako hata kama lina ukweli ndani yake

Siku zote jitahidi kujaribu vitu vingi na kuwa mdadisi mara kwa mara

Kila unapo lazimisha kujua kitu Ndio njia ya kujifunza zaidi na kuwa bora

Wakati mwingine kuna uwezekano hiko kidogo unachokiweza ndio jibu na njia sahihi zaidi au hata hakuna mwingine anaeweza kama wewe kwa wakati huo!

Ubunifu upo kwenye kujaribu mambo tofauti tofauti na mafanikio yapo kwenye ubunifu…

Hivyo kila kinachokuja upande wako kama hakina madhara makubwa na kinahitaji kufanywa na wewe usikubali kusema siwezi,

Badala yake jitutumue Jaribu kidogo, jifunze na ukiweza uliza wengine kinafanywaje? Ila kamwe usiseme HAPANA.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Sababu 5 Zinazo Sababisha Watu Kutofikia Malengo Yao Nchini Tanzania

Next Post

Tumia Nafasi Uliyonayo Kikamilifu

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next