Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Tumia Nafasi Uliyonayo Kikamilifu

Ukipata nafasi ya kusaidia mtu unapoweza msaidie kwa moyo mmoja..

Ukipata nafasi ya kuonesha uwezo hakikisha unaonesha uwezo wote bila kuogopa

Ukipata nafasi ya kufurahi hata kama ni muda mchache jitahidi kutumia muda huo kufurahia kama vile hutofurahi tena!

Ukiona nafasi ya kufanya jambo hata kama ni dogo basi lifanye kwa ubunifu wako wote,

Ukiwa na nafasi yakuwa na familia yako, ndugu jamaa na marafiki basi itumie kwa ukamilifu wake wote

Fanya hivyo kwasababu maisha hayatupi nafasi zaidi, kuna uwezekano mkubwa nafasi uliyopata leo usiipate tena kesho

Hatujui kesho yetu wala hatuna uhakika wa sekunde ijayo..

Lolote linaweza kutokea wakati wowote hivyo tunapaswa kuishi kwa tahadhari na kuyachukulia mambo katika upande Chanya bila kubeba maumivu wala kusababisha maumivu kwa wengine.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Usiogope Kujaribu

Next Post

Usiruhusu Hofu Ikukwamishe

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.