Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Anza Kujisamehe Wewe Mwenyewe Kabla Hujasamehe Wengine

Jisamehe wewe mwenyewe kwanza kwa makosa mengi uliyo jikosea zamani

Jisamehe kwa kosa la kuishi kwenye maisha ya watu wengine wasiokupenda na kuona thamani yako

Jisamehe kwa kutojipa kipaombele na kuwapa wengine kwa lengo la kuwafurahisha

Jisamehe kwa kujiacha nyuma, kutofurahia pesa zako na kujifurahisha kwa sababu ya watu ambao leo hii hawajakulipa wema wowote

Jisamehe kwa ahadi zote ulizojipa lakini ukashindwa kabisa kuzitekeleza wewe mwenyewe kwa sababu yoyote

Jisamehe kwa kupoteza muda kufuatilia mambo ambayo hayaja kujenga mpaka sasa wala kukusaidia chochote

Jisamehe kwa mipango yote uliyopanga kwa ajili yako lakini ukaishia njiani kisa kutoona matokeo mapema

Jisamehe kwa malengo yote uliyoweka Ila bila sababu yoyote ukagairi kuyatekeleza

Jisamehe kwenye kila kitu hata kama hukusababisha wewe au kuna sababu za msingi sana zilikukwamisha

Ukimaliza kujisemehe jiambie kuanzia sasa

SITOKUBALI KURUDIA MAKOSA YANGU TENA

Kisha anza upya ukiwa na imani na nguvu kubwa moyoni

Na wakati huu fanya kweli huku ukiogopa kurudia yale yale uliyoyafanya zamani

Rekebisha maisha yako kwa kuanza na wewe mwenyewe kabla ya kulaumu wengine.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Sio Kila Mlango Uliofungwa Pia Umelokiwa

Next Post

Maisha Sio Kombolela Ila Kuna Watu Wanabutua

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Usiogope Kujaribu

Usiogope kujaribu jambo hata kama unahisi huliwezi au ni gumu sana Kataa kabisa neno haiwezekani kwenye akili…

Huruhusiwi ku copy makala hii.