
Sio lazima utumie nguvu kubwa sana kutaka kuonekana mshindi!
Kuna muda ukimya wako tu unatosha kummaliza adui yako
Sio kila jambo linataka majibizano wala mapigano ya nguvu..
Sio kila kitu lazima kikuchukulie muda wako
Kuna vitu vinapaswa kuachwa kama vilivyo
Kuna washindani wanapaswa kuachwa kama walivyo
Kama jambo halimalizi afya yako wala haligusi moja kwa moja kipato chako Acha lipite!
Kuna wakati unaweza kujikuta unapambana na mtu ambae furaha yake ipo kwenye ugomvi
Kuna muda utajikuta unaumizwa na mtu ambae furaha yake kukuona unaumia
Usikubali kumpa mtu mwingine furaha wakati huo huo unaumia wewe mwenyewe
Acha lipite kwa ajili ya amani ya moyo wako
Ukiwa na amani huwezi kukosa kitu chochote hapa Duniani
Amani Ndio daraja la afya bora na afya Ndio msingi wa mafanikio!
Jifunze kukaa kimya na kuacha mambo madogo madogo yapite kama yalivyo
Ukimya wako ni silaha kubwa kwa adui ambae amejipanga kugombana na wewe
Adui aliyejipanga kukuharibu kiakili mjibu kwa ukimya wako
Mshindani aliyejipanga kukuchafua jina, mjibu kwa ukimya wako
Acha asili iamue, Acha maji yafuate mkondo wake
Kama una uhakika unafanya jambo sahihi bila kuwa chanzo cha changamoto mlizonazo basi chagua upande wa amani yako kuliko ushindi wake.