Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Kwenye Maisha Hakuna Anae Wahi Wala Anae Chelewa

Kwenye maisha kila mmoja yupo katika nyakati zake na muda wake sahihi

Usijione umechelewa sana ukahisi Mungu amekusahau

Usikose raha kisa mafanikio ya mtu mwingine aliyekutangulia

Kumbuka kutangulia sio kufika wala kuchelewa sio kukosa!

Maisha yana mzunguko wake kwa kila mtu, hakuna bingwa sana wala mjinga sana

Unaweza kuchelewa kupata lakini ukapata kilicho bora zaidi

Au hata ukadumu nacho miaka mingi zaidi,

Mwingine anaweza kutangulia kupata na akakipoteza ndani ya muda fulani au akapata kisicho bora kama chako

Kuna watu wametangulia kuoa au kuolewa Ila wakaachika

Kuna watu walipata kazi mapema na wakafukuzwa au kupoteza nafasi zao

Kuna ambao waliotangulia kupata watoto lakini wakawapoteza au hata kuteseka na uzao wao

Kuna wale waliowahi kupata pesa na wakafirisika!

Usisahau kuna ambao walikuwa watu wa dini sana na wakaishia kutenda maovu

Hivyo usiyaonee tamaa mafanikio ya mtu mwingine kabisa

Usijione upo mbali sana na wale walio mbele yako

Kama unafanya jitihada kila siku za kusogea unapotaka basi usiumizwe na muda wala usijilinganishe kama wengine

Fanya jitihada zako kwa kujilinganisha na ulipotoka yaani jana yako

Muombe Mungu akusaidie na akuzidishie kiwango cha imani bila kusahau subra

Najua kuna muda unapitia nyakati za kukata tamaa

Sio rahisi kuona wengine wapo mbele na wewe nyuma kila siku

Inaumiza sana na hata kukufanya uone kama maisha si kwa ajili yako

Lakini subiri wakati wako hakika utasahau maumivu yote unayopitia na utashangaa hata kwanini ulitamani maisha ya wengine.

Mwajuma Muhasu
Lifewithmuhasu.com

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Usikubali Furaha Yako Imilikiwe Na Mtu Mwingine

Next Post

Usihangaike Na Ulivyopoteza Zingatia Vilivyobaki

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.