Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Samaki Mmoja Akioza Muweke Pembeni

Kuna watu wengi sana walikariri ule msemo wa samaki mmoja akioza basi wote wameoza

Hii imefanya watu kupoteza mambo ya muhimu sana kwenye maisha yao

Kwa kulinganisha msemo huo wa wazee kwenye maisha halisi!

Si kila msemo unafaa kutumika kwenye maisha ya kila siku

Mfano huwezi kusema wanaume wote wanafanana tabia kisa mwanaume mmoja au wengi walio kuumiza

Au wanawake wote wapo vile vile kwa matendo yao kisa mwanamke alokutenda

Na hata marafiki wote ndivyo walivyo wapo kimaslahi tu na wanafiki, kumbuka sio marafiki wote wapo hivyo

Au tuseme kundi la watu fulani wote wahesabike kwa makosa ya mwenzao mmoja! Labda kundi la marafiki wa mwizi fulani

Ukiona jambo moja limeharibika toa weka pembeni endelea na mengine

Lakini hata samaki yule yule aliyeoza anaweza kuwekwa viungo na akabaki na utamu ule ule wa mwazo!

Inategemea na utundu wa mapishi tu!

Kwa maana kuwa mtu au kitu kinaweza kuharibika na kikatengenezwa upya! na hata watu hurekebishika

Sio kila jambo linapaswa kuhukumiwa kama lilivyo au kwa makosa ya watu wengine

Kuna vitu vipo kwenye mazingira yasiyo faa kabisa lakini havina uhalisia wa mazingira vilivyopo

Jifunze kutumia busara na akili kwenye kuchanganua mambo na hata kufanya maamuzi sahihi

Bila kulinganisha mambo ya kusadikika na uhalisia uliopo

Yaani usiishi kwa mazoea na kukariri mambo yale yale kila siku

Kuna wakati utapoteza vitu au watu wa msingi kwa sababu za kukariri tu.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Mafanikio Ni Kama Mimba, Kila Mtu Hukupongeza Akiona Tumbo Kubwa

Next Post

Kama Una Smartphone Na Unasema Huna Mtaji, Jitafakari Upya

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.