Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Mafanikio Haya Ambukizwi Kwa Ngono

Hakuna namna yoyote ile kwamba ukiwa kwenye mahusiano na mtu mwenye mafanikio na wewe utapata

Hakuna muujiza wa kuwa kwenye mahusiano na tajiri kisha na wewe akakuambukiza utajiri wake

Hakuna jinsi yoyote ya kuwa na mtu mzito sana au mkubwa sana au kiongozi wa juu sana halafu na wewe akakuambukiza ukubwa na uzito wake kwa njia ya ngono

Kuna watu wengi walioana na watu wenye mafanikio makubwa mno Ila wakaachika au kutengana wakiwa makapuku kama walivyo enda

Kuna wengine walipoteza wenza wao waliokuwa na mafanikio makubwa sana na wakabaki mafukara baada ya muda mfupi sana

Kuna wale walikuwa au wapo na wenza wenye pesa nyingi sana mpaka sasa lakini hawana kitu chochote wanacho miliki wao binafsi

Bila kusahau wapo wanao pewa kila kitu hata mitaji mikubwa na wenza wao na bado hupoteza yote!

Ijapokuwa wapo walio bahatisha kupata mafanikio makubwa kupitia mwenza wao bila jitahida kubwa sana za pembeni, ambapo ni kama kucheza kamari na kusubiri bahati nasibu au usafiri wa meli Airport.

Kuwa na tajiri kwenye mahusiano ni jambo moja na kutajirika kupitia yeye ni jambo la pili

Mafanikio ni pamoja na matumizi sahihi ya akili, jitihada na mchakato wa aina fulani tukiondoa uwezo wa kuwa na pesa za kufanyia kitu!

Kuwa na mtu mwenye mafanikio ni moja kati ya njia inayo ongeza uwezekano wa kufanikiwa…..

Wakati huo huo jitihada za akili za pembeni zikihitajika.

Kupoteza muda kuwa na tajiri au kunyanyasika kisa upo na tajiri kwa matarajio ya kuwa tajiri huku huna mkakati wowote wa ziada ni moja kati ya kujikosea heshima na haki zako za msingi hapa Duniani

Ukiamua kuwa na tajiri kwa sababu zingine ni sawa Ila usitarajie kuambukizwa utajiri wake kimiujiza nje ya jitihada zako binafsi.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Jifunze Kuwapa Wengine Ushirikiano Wanapo Amua Kubadilika

Next Post

Wakati Mwingine Muombe Mungu Ujasiri Na Roho Ngumu Pekee

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.