Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Jifunze Kuwa Jeshi La Mtu Mmoja

Watu wote wanao kuzunguka kuna siku watakuacha!

Wale wanao onesha kukupenda sasa, kuna siku watakuacha!

Wale wote unao ona mnakula bata na good times sasa, ipo siku hutowaona kabisa

Hao ambao wanakuambia maneno mazuri muda huu, kuna siku hutopata hata salamu zao!

Maisha huleta na kuondoa watu kila wakati

Kama hujihisi kukamilika bila kuzungukwa na watu basi wewe ndio tatizo lenyewe!

Haijalishi una sababu za msingi kiasi gani, jifunze kuishi na kujitegemea mwenyewe

Wakati wa shida na wakati wa raha, zoea kuwa mwenyewe

Jipe furaha muda wa mazuri na jipe kumbatio la faraja wakati wa shida

Ukiwa na mazoea ya kuwa mkamilifu bila kuwa na wapambe pembeni maisha yatakuwa marahisi sana kwa upande wako siku zote

Elewa kuwa ulizaliwa mwenyewe na utazikwa mwenyewe

Yaani Mungu mwenyewe anajua kuwa kila mmoja anaweza kuwa peke yake na hakuna tatizo katika hilo

Changamoto huja pale unapotaka kukumbatia kila mtu wakati wote

Sio vibaya kuwa na watu Ila ubaya huanzia pale unapotaka wabaki upande wako nyakati zote!

Jifunze kuwa mwanajeshi na jeshi la mtu mmoja, peke yako unatosha kukamilika

Huhitaji mwingine wa karibu kukufanya ucheke, ulie wala ustarehe.

Watu wamejaa kila mahala utakapo enda, ukihitaji kampani za muda zipo kila sehemu

Sio lazima kuwa na watu kwapani ambao wanajua undani wako na kila unachopitia ndio ujione kama umetimia!

Nenda popote na furahia maisha yako mwenyewe, wakija acha waje na wakiondoka acha waende

Kitu cha msingi ni kuwa iwe wapo au hawapo bado hakuna kitakacho pungua kwako.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Wakati Mwingine Muombe Mungu Ujasiri Na Roho Ngumu Pekee

Next Post

Jifunze Kusema Hapana Usiwe Maharage Ya Mbeya

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.