Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Jifunze Kusema Hapana Usiwe Maharage Ya Mbeya

Watu wengi mno wanateseka kwenye maisha kwa mambo madogo madogo sana

Mambo ambayo yako ndani ya uwezo wao wenyewe na wanalimudu bila shida

Neno HAPANA ni dogo mno Ila limeharibu malengo na ndoto za watu wengi mno Duniani

Ile hali ya kuwa maharage ya mbeya hata kwenye vitu visivyotaka urahisi wako

Kuna vitu sema hapana haijalishi ni kwa mtu, watu au kitu

Usiogope matokeo yatakavyokuwa baada ya kukataa

Ikiwa kitu hakipo ndani ya uwezo wako, wala hakina faida na wewe sema HAPANA

Endapo jambo linaenda kuvuruga bajeti zako na mfuko wako sema HAPANA

Endapo kitu kinaenda haribu akili yako na hata kukupa msongo wa mawazo kikatae kwa nguvu

Ikiwa unaona ratiba zako zitavurugika na kukutoa nje ya mipango kataa kwa nguvu kubwa

Usiogope kuchukiwa wala kusemwa vibaya kamwe kisa kusema hapana

Binaadamu hawaridhiki hata uwape nini, watakusema tu

Mtu akiamua kuona mazuri yako atayaona tu hata kati kati ya mabaya uliyonayo

Na mtu akiamua kuona mabaya yako haijalishi uwe mwema kiasi gani atakuchukia tu

Ipe nafsi yako uhuru na amani kwa kuongeza uwezo wa kusema HAPANA

Jizingatie kwanza wewe kabla ya wengine

Furahia muda wako kabla ya kuugawa kwa wengine

Furahia pesa zako kabla ya kuzigawa kwa wengine

Acha wakuchukie, acha wakuone mbaya, acha wakusema vibaya hilo sio jukumu lako

Zingatia amani ya nafsi yako, zingatia maisha yako, zingatia muda na kipato chako

Ishi maisha unayoona yanafaa bila kuzingatia watu au vitu vingine utaumia bure

Siku utayo weza kusimama na kusema hapana bila hofu wala uoga, Ndio siku utakayo anza kuishi Rasmi

Hakuna raha kwenye maisha kama uwezo wa kukataa bila kuogopa mtu au mazingira.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Jifunze Kuwa Jeshi La Mtu Mmoja

Next Post

Sio Kila Jambo Linapaswa Kutolewa Maelezo Ya Ziada, Usipoteze Muda Wako

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Jifunze Kushukuru

Kadiri unavyo shukuru Ndivyo unavyojisogeza karibu na mafanikio yako Jifunze kuwa na moyo wa kuyaona mazuri…

Huruhusiwi ku copy makala hii.