Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Sio Kila Jambo Linapaswa Kutolewa Maelezo Ya Ziada, Usipoteze Muda Wako

Kuna vitu hupaswi kutumia nguvu kujieleza sana kwa mtu

Yapo mambo hayafai kabisa kutolewa maelezo ya ziada ili yaaminike

Kuna matukio hata hayapaswi kutolewa sababu za kwanini yanafanyika au yalifanyika

Halafu zipo nyakati huhitajiki kufungua mdomo wako kabisa zaidi ya vitendo tu, jibu moja au maneno machache tu

Ukijiona bado unajieleza sana kwa watu kisa kitu fulani…

Ukijiona bado unapaswa kutoa maelezo mengi ya kujitetea…

Kama upo kwenye kundi la kuhitajika ushahidi au shuhuda ili uaminike…

Tambua bado hujaanza KUISHI

Na mbaya zaidi hayo hayo maelezo unayotoa ndio chanzo cha kudharaulika zaidi.

Kwenye Haya maisha haijalishi utawaeleza watu mambo mangapi ya kweli au uongo

Kama mtu kaamua kuona kitu fulani ni bluu hata kama ni nyekundu, elewa kamwe huwezi badili akili yake

Kuna mtu akisha amini kitu hata kama alisikia uvumi bila uhakika basi tayari humtoi kwenye imani yake

Kuna mtu atajifanya anataka kujua ukweli kumbe pembeni ana ku ng’ong’a

Kuna mtu hutaka maelezo lakini kwenye akili yake tayari ameshafanya maamuzi mengine

Sio kila mtu anapaswa kukulia muda wako wa maelezo

Usipoteze muda na nguvu kutoa maelezo ambayo mwisho wa siku hayata badili chochote!

Toa maelezo sehemu kwa lengo la kujenga kitu bora zaidi

Jieleze pale penye faida na panapo lenga kukuingizia zaidi

Mengine yote ambayo hayana maana kwako wala kwenye maisha yako hayapaswi kukuchukulia muda wako wa maelezo

Acha waelewe kwa namna wanayotaka kuelewa

Acha waamini wa nachotaka kuamini

Ikiwa hakuna madhara ya moja kwa moja yatajitokeza kwako!

Mwisho wa siku muda sahihi ukifika ukweli hujitenga na uongo hujitenga hivyo acha muda uongee,

Kujenga heshima yako binafsi ni pamoja na kupunguza kujieleza sana au kutoa sababu kila wakati.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Jifunze Kusema Hapana Usiwe Maharage Ya Mbeya

Next Post

Kuna Muda Tumia Neno Liwalo Na Liwe

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.