Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Kuna Muda Tumia Neno Liwalo Na Liwe

Kuna zile nyakati umeandaa kila njia na ipo sawa

Umefanya kila unachoweza na kipo sawa

Umetoa kila ulichonacho na huna ulicho bakiza

Umetumia mbinu zote na huna mashaka kabisa

Kila ulicho paswa kufanya umefanya kwa uhakika wote

Kila ulicho hitajika kutimiza umetimiza vyote

Majukumu ya upande wako yote yapo sawa na huoni kabisa kilichopungua

Kiufupi huna deni lolote wala majuto ndani yako

LAKINI HUONI MATOKEO WALA MABADILIKO YOYOTE!

Haijalishi ni kwenye kitu gani, iwe biashara kazi masomo au mahusiano au mambo mengine yoyote yale.

Basi ni wakati sahihi sasa kutumia neno LIWALO NA LIWE

Usijiumize kichwa sana wala kuwaza sana na hata kulaumu sana

Usione kama una mapungufu, huna nyota au hata una laana fulani

Usihisi kama vile umerogwa au hata Mungu amekusahau na kukuona huna maana kwake.

Kila jambo huja kwa wakati wake hivyo fanya unachopaswa kufanya na mengine acha muda uamue

Hupaswi kulaumu na kuhisi kama kuna mapungufu fulani ndani yako

Usijidhuru wala kujisababishia matatizo yasiyo na msingi wowote.

Fanya kwa kiasi chako, uwezo wako na kisha acha muda uamue matokeo yako

Neno LIWALO NA LIWE hupunguza maumivu, huondoa msongo wa mawazo na kuponya moyo wenye majonzi

Lakini pia ni dawa ya moyo na akili kushusha mzigo mzito uliobebwa kwa ndani

Ukiwa na mazoea ya kutumia neno hili mahala sahihi kwa wakati sahihi ni tiba kubwa sana na huleta mabadiliko makubwa mno kwa mtu na maisha kwa ujumla

Ila hakikisha umefanya kila ulichopaswa kufanya, Pumua kwa nguvu kisha funika kila kitu na sema neno LIWALO NA LIWE, Kisha ngoja matokeo yoyote na yapokee.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Sio Kila Jambo Linapaswa Kutolewa Maelezo Ya Ziada, Usipoteze Muda Wako

Next Post

Kama Upo Katikati Ya Giza, Usisimame Wala Kurudi Ulipotoka Kisa Uoga, Songa Mbele

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.