Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Usisahau Kuishi Wakati Unatafuta Maisha

Wakati unahangaika kutafuta maisha yako unayotaka

Ndio wakati huo huo pia unapaswa kuishi maisha unayotaka

Kila kilicho original kina kopi yake na kila kilicho kamilika kina summary yake

Hivyo unaweza kugeuza maisha unayotaka kuishi baadae, ukayaishi sasa kwa namna tofauti!

Usingoje mpaka umiliki vitu fulani ndio ufurahie maisha yako

Furaha hupaswa kuwa sehemu na mazoea ya maisha unayoishi kila siku haijalishi kiwango cha mafanikio uliyonayo

Ishi wakati unatafuta maisha, usisubiri kitu chochote

Badili mtazamo wako kwa namna tofauti na utaona muujiza mkubwa sana wa raha ya maisha

Kuna watu wana mafanikio makubwa Ila hawana amani wala raha ya mafanikio yao

Watu hao hao kabla ya kufanikiwa walisema, “siku nikipata mafanikio fulani nitakuwa na furaha sana”

Ajabu ni kuwa mafanikio wamepata Ila furaha na amani hawana kabisa.

Kuishi wakati unatafuta maisha yako ni neno lenye maana pana sana

Lakini kwa ufupi ni kuwa hakikisha kila giza linapoingia uwe umekamilisha maana ya siku nzima uliyoishi siku hio

Jitahidi kabla hujalala ujione kabisa siku yako imeenda vile umetaka na huna deni na maisha yako kabisa

Lakini pia jitahidi umiliki furaha yako bila kujali changamoto unazopitia

Na usisahu kujipa raha kwenye hiko hiko kidogo unachopata

Wala usiendekeze shida na mahitaji ya maisha maana huwa haviishi kamwe!

Ishi maisha makamilifu unayotaka kuyaishi bila kujali kiwango cha mafanikio yako

Ukipata muda wa kufurahia basi furahia kama vile hutofurahi tena

Na ukipata nafasi ya kutumia basi tumia, jiachie kama vile tayari umemaliza shida zako zote, Ila hakikisha huharibu bajeti yako!

Sio lazima uwe serious sana na maisha, hujaumbwa kuteseka

Hata Mungu hufurahi na kutoa zaidi kwa wale ambao huonesha hali ya kuridhika na kufurahia kidogo wanachopewa!

Badili matazamo wako hakika Dunia ni sehemu tamu sana.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Kifo Hakina Taarifa, Jiandae Mapema

Next Post

Kubali Uhalisia Kuna Mambo Hayabadilishiki

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.