Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Mungu Hakuumba Binaadamu Kwa Uwezo Mkubwa Awe Mzururaji

Mungu hajaumba viumbe wake hususani binaadamu,

Kwa uwezo mkubwa sana kisha binaadamu huyo huyo aje kuzurura kisha kufa

Mungu ameumba binaadamu kwa maarifa mengi sana sio kwa lengo la binaadamu huyo kuzurura na kufa

Furaha ya mungu sio binaadamu wake kuwa mzururaji haijalishi ataishi kwa miaka mingapi Duniani

Tukiondoa wale ambao hufa mapema kabla ya umri wa kujiambua,

Wengine wote wanapaswa kufanya kitu kwa ajili ya Mungu wao!

Kama una miaka zaidi ya 18 sasa una afya njema na huna ulemavu mkubwa wowote basi tambua una deni kwa aliyekuumba.

Uliwashinda ndugu zako wengi wakati mbegu yako ikikimbia kulitafuta yai la mama ndani ya via vya uzazi

Maana yake uliweka mkataba na Mungu kuwa wewe ni bora kuliko wengine na ukapewa nafasi ya kuumbwa

Wengine wote wakatolewa nje kama uchafu na wewe kama kiumbe

Sasa kwanini bado una kubali kuwa mzururaji?

Kwanini una kubali kupoteza muda kulala ndani kwako?

Kwanini hutaki kabisa kufikirisha akili yako?

Kwanini unaleta uvivu usio na maana wakati una uwezo wa kubadili historia yako?

Kwanini bado una kesha nyumba za ibada kuomba msaada kwa Mungu wakati tayari amekuumba na kila kitu?

Abudu kwa kushukuru na kumtukuza Mungu sio kila siku kulilia shida ambazo hazina mantiki

Kuna watu wana kila sababu za kumlilia Mungu wao Ila sio wewe!

Shtuka usingizini pambania hatma yako kwanza

Muoneshe Mungu upo tayari kusimama na kumtukuza kwa vitendo

Vitendo vya upambanaji na nia ya kujikwamua kwa vitendo halisi

Kisha Mungu ataweka mkono wake katika jitihada zako.

Mfanye Mungu ajisifie kwa kile alichokiumba kupitia maarifa unayotumia Duniani

Mfanye Mungu afurahie na oene matunda ya uumbaji wake

Mfanye na yeye aseme Hakika sikupoteza muda kuleta kiumbe wa mfano wangu.

Sasa kiumbe wa mfano wa Mungu nae anakesha kumlilia Mungu ampe mkate wa siku pasi na jitihada zozote! Hakika ni maajubu makubwa sana ya Dunia.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Binaadamu Husahau Mema Haraka, Usijimalize Sana

Next Post

Kisasi Kizuri Zaidi Ni Kuwa Bora Zaidi Ya Mwanzo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Kula Kondoo Aliyenona

Kama umeamua kula kondooo kula aliyenona haswaaa, Kiasi kwamba hutojutia kabisa hata kama alikuwa kondoo wa wizi…

Huruhusiwi ku copy makala hii.