Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Kisasi Kizuri Zaidi Ni Kuwa Bora Zaidi Ya Mwanzo

Kama unataka kulipa kisasi kizuri sana chenye akili kubwa na kinachouma zaidi

Basi kuwa bora zaidi ya ulivyokuwa awali!

Hakuna kisasi kizuri ambacho huumiza mtesi au adui yako kama kukuona umefanikiwa zaidi ya mwazo

Hakuna kisasi kitamu ambacho humnyima usingizi adui yako kama kukuona umepiga hatua zaidi

Achana na mambo ya kurogana au kuumizana maana kuna uwezekano mkubwa ukaumia wewe zaidi

Usipoteze muda, nguvu na pesa zako kumuumiza adui yako yoyote

Kwasababu utajiumiza wewe mwenyewe na pengine kumpa yeye sababu au furaha zaidi

Adui yoyote lengo lake kubwa ni kuona unateseka au unaharibikiwa zaidi

Sasa akiona mambo yameenda tofauti, humfanya akose raha na kujiona mjinga

Hivyo basi huna sababu za kugombana na mtu wala kurushiana maneno

Ikibidi usitake hata kujua atafanya nini baada ya yote hayo kiufupi msahau na mpuuze kwa muda

Weka pamba sikioni kabisa, ikibidi vaa mawani meusi na jifanye huoni kitu

Na hata badilisha kila unachoweza na kisha wekeza nguvu, pesa na maarifa yote kuwa bora kuliko awali

Badili matazamo wako wote, hamisha nguvu zako zote na weka akili yako kwenye mambo yanayo kujenga zaidi

Hamishia hasira zako zote kwenye maisha na malengo yako muhimu

Gombana na ndoto zako kwanza kabla hujagombana na yoyote

Lilia malengo yako kwanza kabla hujatoa chozi kisa adui na mtesi wako

Weka visasi kwenye malengo yako binafsi yaliyo kwama kwanza kabla hujataka kulipa kisasi kwa adui yako

Tukana malengo yako ambayo hayaja fanikiwa kwanza kabla hujatukanana na adui yako

Kiufupi adui yako wa kwanza yawe malengo na ndoto zako

Yashinde malengo yako kisha adui wa pembeni utakuwa umemshinda kuliko unavyodhani

Utamuua adui yako halisi akiona mafanikio yako kwa mbali huku yeye akiwa amebaki vile vile

Hakuna kitu kinauma kama mtu akujibu kwa vitendo vya mafanikio zaidi.

Kwahio kuanzia sasa usigombane na mtu ugomvi usio na mashiko

Gombana na maisha yako kisha adui yako atajimaliza yeye mwenyewe kupitia maumivu ya mafanikio yako.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Mungu Hakuumba Binaadamu Kwa Uwezo Mkubwa Awe Mzururaji

Next Post

Kufa Na Tai Shingoni Kwenye Baadhi Ya Shida Zako

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.