Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Kama Ndoa Haikupi Heshima Wala Nafasi Ya Kupigania Malengo Yako, Hio Haifai Kuwa Ndoa

Usichanganye kati ya sheria za Mungu na uoga wako wa maisha

Usihusishe kabisa mila na tamaduni kisa uoga wako mwenyewe

Wanawake wengi sana wanateseka mno kwenye ndoa zao kwa kisingizio cha Mungu

Wengine huogopa macho ya watu, ndugu mila na tamaduni zao

Sio kwamba wanapenda kukaa kwenye ndoa walizopo!

Mama yangu alikuwa muhanga wa ndoa za maumivu na mateso

Alikaribia kunisababishia kifo kisa ndoa yake

Mara baada ya kuachana na baba yangu mzazi, jamii ilimuandama sana

Eti kwanini aliomba talaka yake! Licha ya kupitia mateso kwa baba yangu

Yani walitaka avumilie mateso kisa mwanamke hupaswa kuwa mvumilivu!

Kwahio baada ya kuachika alitafutiwa mume mwingine na akaolewa kwa nguvu

Yule mume alikuwa na wake wengine 2 pamoja na mama jumla wanawake 3

Maisha ya yule mwanaume yalikuwa magumu sana kama mnavyojua mashekhe au tuseme walimu wa madrasa

Alikuwa na wake 2, watoto zaidi ya 15 na hali duni sana ya maisha

Na bado hakutaka mke wake yoyote afanye kazi au biashara yoyote ile

Kula ilikuwa mara1 tu kwa siku tena chakula tuligombania kama sandakalawe! na mwenye nguvu pekee ndio angalau hupata ujazo kidogo wa shibe

Mama alikuwa muhanga wa mateso ya ndoa kuanzia kwa mume mpaka wake wenzake kama mnavyojua ndoa za mitala

Ila aliogopa kuachika kwasababu ya macho ya watu na vitisho vya wazazi na ndugu zake!

Kuna siku niliumwa sana homa kali mno, baada ya kupelekwa hospitali na kuandikiwa dawa mama hakuweza kununua

Gharama ilikuwa elfu 1000 tu za kitanzania Ila hakuwa hata na mia nyekundu wala mume hakutoa msaada

Kama mnavyojua hospitali za serikali dawa utaambiwa zimeisha licha ya kuwepo!

Hivyo mama alirudi akiwa na mawazo mengi mno huku hali yangu ikiwa mbaya sana

Ndio akapata mawazo ya kuomba msaada kwa babu yangu aninunulie dawa

Ila babu (upande wa ubabani kwangu) aliamua kuni chukua na kunilea kisha yeye kubaki kwenye ndoa yake

Yani mama alikaribia kunipoteza kisa ndoa! Au tuseme uoga wa kuachika endapo angefanya biashara yoyote kujikwamua

Mama alikaribia kuniua kwa homa kisa ndoa yake na macho ya watu waliomsimanga kwanini aliachika ndoa ya kwanza!

Mama angesababisha kifo changu kisa ndoa ambayo haina msaada wowote ule

Au tuseme sheria ya Dini inataka mwanamke amtii mume wake je, ningekufa Mungu angelipokea katika namna gani hilo?

Je, mama yangu angebaki anasema nimekufa kwa Mapenzi ya Mungu au angejilaumu kwa kufuata sheria za dini yake?

Wakati mwingine madhara mengi hutokea kwa watu kufuata sheria ambazo hazina uhalisia

Uoga wa kusemwa au kwenda nje ya mila na tamaduni zimepelekea vifo vya watu wengi sana

Wanawake wanaishi kwa kufuata Kauli za wanaume zao, Kauli ambazo huua ndoto na malengo yao kisa ndoa!

Ndoa zimejaa maumivu na machungu mengi mno kila kukicha

Ila wanaogopa kutoka au kusema kisa watapoteza wanaume kana kwamba hao wanaume ndio pumzi zao.

Shtuka! Kama ndoa haina heshima wala kukupa nafasi ya kupigania malengo yako, hio haifai kuwa ndoa.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Usimsaidie Mtu Msaada Ulioficha Manyanyaso Kwa Ndani

Next Post

Dunia Ina Mambo Mengi Sana, Chagua Yako Machache

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.