Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Maisha Sio Mashindano, Shindana Na Jana Yako

Maisha sio sehemu ya kushindana kati ya mtu na mtu mwingine kwenye mafanikio aina yoyote

Haijalishi unataka mafanikio kwa kiwango gani, kamwe hupaswi kushindana na mtu

Kama unataka mashindano basi shindana na jana yako

Shindanisha mwaka wako huu na mwaka wako uliopita

Shindanisha mwezi wako huu na mwezi wako uliopita

Lakini pia shindanisha mafanikio uliyonayo sasa na mafanikio yako yaliyopita

Kamwe huwezi kuwa na furaha ya dhati kama utataka kumshinda kila mtu kwa sababu kadiri utakavyo pambana kuwa juu, kuna mwingine pia atataka kuwa juu yako zaidi

Hivyo utapoteza muda mwingi kutaka tena kuwa juu ya yule na pengine usiweze kabisa, muda ambao ungetumia kufurahia maisha yako!

Jambo la msingi zaidi unapaswa kuwa bora kuliko ulivyokuwa awali

Kama una maisha yanayokupa furaha, una vitu muhimu na bado unapambana kuwa bora zaidi, basi inatosha.

Hupaswi kuwa mvivu wala hupaswi kushindana na mtu yoyote yule

Kwani watu wana siri nyingi mno kwenye mioyo yao na wala huwezi jua wanayo pitia!

Pengine mtu unaekesha kutaka kushindana nae, na yeye kwa siri anakesha kutaka kukukomoa!

Au yule unaehisi ni bora na amejipata sana, kumbe nyuma ya pazia anapitia magumu na mazito mengi

Pia usisahu kuna wale ambao kwa nje unaona wamefanikiwa mno Ila kwa ndani yao wanatamani kuwa na maisha kama yako!

Ndugu yangu kamwe kamwe kamwe usiwe mtumwa wa mafanikio ya wengine

Usiumie kisa maisha na mafanikio ya mwingine haijalishi anaonekanaje kwa nje

Komaa na pambana kuboresha maisha yako wewe mwenyewe kwa njia zako

Angalia jana yako kisha utajua kama umefanikiwa au umerudi nyuma

Kumbuka kuna uwezekano mkubwa una maisha mazuri sana kuliko hao wengine unao watazama kwa nje.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Hujaumbwa Kuteseka, Mateso Unajisababishia Wewe Mwenyewe

Next Post

Chunga Njia Unazopita Sasa Kusaka Mafanikio, Zisiwe Na Mwiba Kwenye Maisha Yako Ya Baadae

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.