Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Kuna Kumbukumbu Za Maisha Hazina Ufutio, Chunga Tamaa Zako

Usikubali kabisa tamaa na mapito ya maisha, zikufanye ubaki na kilema cha kudumu

Kuna mambo hayabadiliki hata kama yatasahaulika kwa muda

Kuna mambo hayafutiki hata kama utatumia ufutio wa gharama kubwa sana kufuta

Na kuna vitu alama zake hutengeneza kumbukumbu za milele tena za kudumu!

Leo hii unaishi vile unataka na una kiburi cha kufanya jambo lolote lile kwa kisingizio cha maisha

Ila kuna siku utatamani kuishi maisha tofauti na hayo ya sasa

Utapata wito na maoni ya kuwa aina nyingine ya mtu tofauti kabisa

Utapata nafasi kubwa zaidi au hata fursa nzuri na kubwa zaidi ya ulivyo sasa

Ila kumbukumbu na matukio mengi ya nyuma yatakukwamisha!

Utatamani kufuta kila kitu, kisha kuanza upya na hutoweza tena!

Utataka hata kurudisha siku nyuma na uanze upya, Ila hutoweza tena!

KUMBUKA :

Tamaa za muda mfupi zinaweza kukupa maradhi ya kudumu

Tamaa za muda mfupi zinaweza kukupa kilema na alama za kudumu

Tamaa za muda mfupi zinaweza kuvunja heshima yako ulioijenga miaka mingi sana

Tamaa za muda mfupi zinaweza kukutoa kwenye fursa kubwa za maisha yako

Tamaa za muda mfupi zinaweza kukufanya ufungwe kifungo cha maisha

Bila kusahau tamaa hizo hizo zinaweza ondoa uhusiano wako mzuri na watu wako wa karibu

Na vile vile tamaa za muda mfupi sana zinaweza geuza maisha yako kichwa chini miguu juu kwa muda mfupi mno!

Bila kusahau kukuachia kumbuka za kudumu kwako na wanao kuzunguka!

Hivyo chunguza mara mbili maamuzi unayotaka kufanya kabla hata hujachukua hatua

Usikubali tamaa ziwe chanzo cha majuto kwenye maisha yako

Usikubali kupelekwa kasi na tamaa ambazo unaweza kujizuia kwa sekunde chache tu na kutunza utu wa milele

Wala usikubali maamuzi yako mwenyewe yawe sababu ya kujuta maisha yako yote yaliyobaki

Jizuie na jishikilie kidogo, ufundishe moyo wako kuchagua kipi muhimu na kipi chakupuuza.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Chunga Njia Unazopita Sasa Kusaka Mafanikio, Zisiwe Na Mwiba Kwenye Maisha Yako Ya Baadae

Next Post

Usisahu Kujenga Maisha Yako Binafsi, Wakati Unajenga Maisha Ya Familia Yako

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.