Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Kama Huwezi Kujenga, Basi Angalau Usibomoe

Kama huwezi kujenga kabisa, basi angalau Usibomoe

Kama huwezi kutengeneza kabisa, basi usiharibu

Kama huwezi kurekebisha, basi usichokonoe

Kama huwezi kujenga hoja, basi usipinge hoja za wengine

Kama huwezi kusambaza nguvu chanya basi angalau usisambaze nguvu hasi

Kama huwezi kuleta furaha kwa watu basi angalau usiwe chanzo cha huzuni zao.

Mambo unayofanya leo hii yana mchango gani kwa wengine!?

Matendo yako ya leo, ni kwa kiasi gani hujenga au kubomoa jamii?

Njia unazotumia kupata pesa, zinajenga au kubomoa jamii?

Maudhui unayoweka mitandaoni, yanajenga au yanabomoa vizazi vya sasa na baadae?

Maneno unayotamka kwenye kichwa chako, yana jenga au kubomoa jamii?

Usiwe mbinafsi sana na kufikiria upande wako pekee

Usiwaze faida yako na ukoo wako kisha ukasahau jamii inayokuzunguka

Kama huna aibu na umeamua kujitoa kufanya unachofanya kwa lengo lako na ndugu zako basi angalau pia kumbuka jamii inayobaki na kudhurika kupitia wewe!

Shida sio njaa ya mafanikio, pesa, Mali au hata umaarufu, shida ni kwa kiasi gani utahusika kubomoa wengine kupitia njia unazotumia kupata unavyotaka

Usiwe chanzo cha majonzi kwa wazazi, ndugu na jamii inayoharibikiwa vizazi vyao kwa sababu ya njia zako Unazopita kutafuta mafanikio

Ni rahisi sana kuharibu vilivyo jengwa na ngumu sana kujenga vilivyoharibika

Leo upo na kesho haupo je mbali na Mali ulizochuma, umaarufu uliopata na mengine yote, unahisi utaacha kumbukumbu gani nyingine yenye mchango Chanya kupitia maisha uliyoishi kwenye jamii yako?

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Umeumbwa Kuitawala Na Kutumikiwa Na Dunia

Next Post

Kimtokacho Mtu Mdomoni Mwake, Ndicho Kilicho Mjaa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Kula Kondoo Aliyenona

Kama umeamua kula kondooo kula aliyenona haswaaa, Kiasi kwamba hutojutia kabisa hata kama alikuwa kondoo wa wizi…

Huruhusiwi ku copy makala hii.