Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Akili Za Kuambiwa Changanya Na Zako

Moja kati ya jambo kubwa zaidi nililojifunza hasa katika maisha ya utafutaji ni

Kuchanganya akili zangu binafsi kwenye akili za wengine

Kuchanganua mambo ninayoambiwa na wengine kabla ya kuamini

Kutokukurupuka na kuamini jambo lolote kabla ya kuchunguza

Kutokuwa kihere here kwenye mambo ninayo ambiwa

Hususani kwenye jambo linalohitaji pesa au linaloenda kuharibu uhusiano wangu kwa wengine.

Kuna watu ni mabingwa sana wa kudanganya wenzao kwa kisingizio cha mjinga ndio aliwao!

Ujinga wako kwenye kitu fulani huwa baraka kwa wengine wapigaji!

Dunia imebadilika sana kila mtu yuko bize kunufaika binafsi bila kujuli maumivu wanayoacha kwa wengine

Hawaoni shida kabisa kuumiza akili, mahusiano na mfuko wa mtu mwingine kwa manufaa yao binafsi

Watakulaghai kwa maneno yenye matumaini makubwa sana na kivuli feki cha mafanikio yao ili uingie mkenge kisha wakulize na kukimbia

Hivyo umakini unahitajika sana hasa pale unapotafuta taarifa kuhusu kitu

Umakini ni muhimu sana hasa pale unapopewa taarifa kuhusu kitu

Umakini ni lazima kwa jambo lolote lile ambalo linatoa pesa yako mfukoni au kuharibu uhusiano wako kwa wengine

Usiwe mtu unae sikiliza na kuamini haraka kila unachosikia au kuona bila uchunguzi

Tenga muda wako kufikiri na ukiweza chunguza zaidi kabla ya kuchukua hatua yoyote hata kama umeletewa ushahidi mezani.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Ukitupacho Wewe Kwa Wengine Ni Dhahabu, Kumbuka Wenye Shida

Next Post

Maneno Hayarudishiki Mdomoni, Chunga Sana Ulimi Wako

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.