Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Maneno Hayarudishiki Mdomoni, Chunga Sana Ulimi Wako

Ni rahisi sana kutamka chochote kile kutoka kwenye kinywa chako

Unaweza kutamka chochote, kwa mtu yoyote na wakati wowote ule kutokana na matakwa yako binafsi,

Lakini ni ngumu sana kufuta kumbukumbu za maneno yako kwenye mioyo na akili za wengine

Unaweza kuomba msamaha na ukasamehewa Ila kamwe msahama haufuti kumbukumbu ya maneno yako kwenye mioyo ya wengine

Mdomo na ulimi ni mwepesi sana kuongea chochote kile kinachokuja kutokana na hisia ulizonazo kwa wakati huo lakini kamwe huwezi badili kumbukumbu za maneno yako kwa wengine.

Kabla hujaongea au kuropoka chochote unapaswa kufikiria madhara yake kwanza

Usijifiche kwenye kivuli cha msamaha kwa sababu msamaha sio ufitio wa madhara ya maneno yako

Unaweza kusamehewa kwa maneno lakini ukaacha alama mbaya sana kwenye mioyo ya wengine

Maneno hayarudishiki mdomoni kwa maana kwamba ukisha ongea tayari umeongea!

Na pia maneno ni ishara ya kile kilicho kujaa kwa ndani yako,

Ni bora umuadhibu mtu hata kwa viboko kuliko kauli mbaya kwa sababu ukali wa maneno mabaya hushinda hata ukali wa upanga!

Kukaa kimya sio ujinga na kamwe huwezi kuchekwa au kuharibu kisa ukimya

Ni bora ukae kimya kama huna kabisa kitu cha kuongea hususani kitu kinacho jenga mahusiano na kuboresha!

Ni bora uonekane mbaya kwa kukaa kimya kuliko kujenga ubaya kisa kauli zako

Hakika ulimi ni adui mkubwa sana wa mtu binafsi, hivyo chunga sana ndimi yako

Licha ya ndimi kuonja ladha ya vyakula, pia kazi nyingine ni kujenga au kubomoa mahusiano na wengine

Uhuru wa kuongea usikufanye ujutie majuto makubwa baadae

Uhuru wa kusema chochote usikufanye uvunje heshima yako

Uhuru wa kutamka chochote usikupe uadui na watu pasi na sababu za msingi

Lakini pia uhuru wa kuongea unaweza kutabiri kiwango cha mafanikio yako ya baadae

Hivyo tumia vizuri uhuru wako wa kuongea na chunga sana ndimi yako ili kujenga kesho yako iliyo bora.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Akili Za Kuambiwa Changanya Na Zako

Next Post

Tumia Mshahara Na Kipato Chako Binafsi Kusapoti Biashara Yako Mpaka Pale Biashara Yako Itakapoweza Kusapoti Kipato Na Maisha Yako

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.