Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Usijione Mjanja Sana Kupata Kabla Ya Wengine, Kumbuka Maisha Hayana Bajeti

Hivi unajua kuwa Kutangulia kwako kabla ya wengine sio sababu ya kufika kabla ya wengine?

Hivi unajua kwamba Kutangulia kwako kabla ya wengine sio sababu ya kupata wa kwanza kabla ya wengine?

Simaanishi kuwa kuchelewa ni kigezo cha kuzingatiwa au kizuri

Na wala simaanishi kuwa hutakiwi kuwahi kufika kabla na unapaswa kuwa nyuma

La hasha!

Nina maanisha kuwa haijalishi umewahi Kutangulia umbali gani kuliko wengine, hio sio sababu ya wengine kuwa nyuma daima

Haijalishi utapata vingapi kabla ya wengine, elewa kuwa nao muda wao ukifika wanaweza kupata kuliko wewe

Haijalishi umepata mafanikio kiasi gani kabla ya wengine, jua tu hata wao wanaweza kupata mwishoni kwa kuchelewa sana Ila wakapata kilicho bora kuliko chako.

Hivyo unapotangulia mbele ya wenzako isiwe sababu ya kujiona mjanja au umepatia sana maisha

Unapopata nafasi ya kuwa mbele ya wenzako usijione mjanja sana na tayari mwendo umeumaliza!

Unapopata baraka yakuwa mbele kuliko wengine, elewa kuwa hata wao kuna siku watafika na hata kukupita umbali zaidi ya uliopo wewe

Hivyo heshimu sana yule unaemuacha nyuma haijalishi umemuacha umbali kiasi gani

Maisha hayapo kwa ajili ya mtu mmoja bali yapo kwa wote wanao yatafuta

Halafu uzuri wa maisha ni kuwa hayana bajeti, (budget) yaani yenyewe hugawa kwa yoyote wakati wowote na hayajawahi kuishiwa!

Hivyo kuwa makini sana na usihisi kama umemaliza budget ya maisha na wengine hawawezi kupata tena

Kwa sababu kuna siku unaweza kushuka chini ukakosa hata mahala pa kuomba msaada

Waswahili wanasema “usitukane mamba kabla hujavuka mto”

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Kuna Wakati Maisha Ni Simulizi Isiyoelezeka

Next Post

Simama Na Hatma Yako, Kwakuwa Hata Waliofanikiwa Waliamua Kusimama Na Hatma zao

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.