Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Urafiki Wa Kweli Hauna Mashaka Wala Kipimo Cha Upendo

Leo nimekumbuka sana maisha ya nyuma na moja kati ya vitu vilivyo nifanya nikumbuke sana ni Rafiki zangu watatu

Kwenye maisha nimewahi kukutana ma watu wengi sana tofauti tofauti

Nimewahi kuwa na urafiki na watu wengi tu tena jinsia na rika aina zote.

Ila nina marafiki zangu watatu ambao waliacha alama kubwa kwenye maisha yangu,

Unajua tumezungukwa na marafiki wengi sana Ila asilimia kubwa huwa nasi kwa ajili ya faida fulani,

Sio kila rafiki ana mapenzi ya dhati kwako

Asilimia kubwa ya marafiki ni wanafki sana hawa ndio wale wakiona umepata huumia mno ndani kwa ndani

Marafiki ambao wanawinda faida tu, siku usipowapa wanachotaka hukubwaga kama uchafu dampo.

  1. GWAMAKA
    Dada huyu sijui nieleze vipi ila alinipenda kwa zaidi ya asilimia 100

Alinipenda wakati sina hata mia, na hakuwahi niomba hata 100 pindi nilipopata maisha

Huyu nimesota nae sana kitaa, enzi hizo hatuna hata pesa ya kula (tumetiana sana moyo kwenye utafutaji)

Nilijua ananipenda Ila sikujua kama ananipenda kwa kiwango kilichopitiliza

Nakumbuka siku ambayo nilifaulu mtihani wa kidato cha 6 (nilienda kumwambia kwake maana tayari alikuwa anaishi na mchumba wake)

Nilivyofika nikiwa nacheka kwa furaha, alihisi tu kuna kitu so nikamwambia nimefaulu mtihani

Aise kwa mara ya kwanza namuona mtu analia machozi ya furaha kwa ajili yangu

Gwamaka hakujibu kitu Ila alibubujikwa na machozi bila kutegemea na ghafla alinikumbatia kwa nguvu sana

Unajua maisha ya urafiki wa uswahili kwanza hatuna mambo ya kukumbatiana, hayo wanafanyaga watoto wa masaki

So ilikuwa mara yetu ya kwanza kukumbatiana halafu pasipo na maandalizi wala kutarajia

Guess how much real friendship feelings ilikuwa pale (yani ile true feelings unahisi kabisa hii imetoka damuni kabisa) mpaka akili ilihama kwa muda!

Gwamaka hata asingenipongeza kwa mdogo yani vitendo tu vilifanya nijue kuwa amefurahia mafanikio yangu kwa moyo wa dhati sana

Nampenda sana Gwamaka she is true friend kwenye shida na raha.

  1. MARIA
    Huyu binti dah sina hata maneno mengi maana alinionesha urafiki wa dhati sana

Nakumbuka siku moja nilichelewa kurudi kutoka shuleni

Unajua kutembea kwa mguu from buguruni to tandika ni bonge la hatua (mbaya sasa mvua ilinyesha kubwa sana siku ile)

Nililazimika kukaa njiani mpaka mvua iishe kwanza maana ilikuwa hatari

Shule nilikuwa natoka sa 1 au sa 2 usiku na mpaka kufika tandika najikuta nafika saa 3 mpaka 4 huko inategemea na namna ntakavyochapulisha miguu.

Maria alikuwa anafunga duka saa 4 kwa ajili ya usalama maana tandika kuna vibaka sana

So siku hio nilijikuta nafika karibia sa 6 usiku (Ajabu nilikuta Maria hajafunga duka mpaka muda ule)

Nilishangaa sana kwanini hajafunga duka (nikawaza labda sababu ya mvua but bado sio sababu kubwa maana vibaka wangeweza vamia kwa wepesi zaidi kutokana na mvua +giza)

Nilifika pale dukani nikakuta Maria kainama, chini ni kama hakuwa Sawa,

Aliponiona alinivamia kwa hasira ni kama alitaka kunipiga kibao but akajizuia

Kwanza nilishangaa sana why yuko vile au nimemkosea Maria!

Wakati naendelea kushangaa na kuwaza haraka nijue kosa langu, ndio akaniambia

“Kwanini umechelewa mpaka muda huu na simu yako haipatikani?” umenifanya nihatarishe kazi sababu yako! Nawezaje kwenda kulala na sijui uko wapi?

Hapo kwanza hata sikuwa nakumbuka kama nna simu (niliizima sababu ya mvua so ilikuwa off kwenye mkoba wangu).

Kabla sijajibu wakati nakagua ili nitoe simu yangu, Maria alinipa sahani ya wali na soda

Eti kwa hasira (Ila najua alinisubiri ili anipe chakula halafu sasa ule wali kumbe aliweka oda kwa ajili yangu mimi na yeye na alitaka tule pamoja)

Dah hahahha kwanza najikuta nacheka maana pia siku ile nilicheka sana

Kumbe hakufunga duka sababu yangu

Maria aliamua kuweka kazi yake hatarini sababu yangu mimi tu

Maria aliamua kupigwa na baridi kwa ajili yangu mimi tu

Maria aliweka maisha yake hatarini usiku wa giza na mvua kubwa sababu yangu mimi tu (imagine vibaka wangevamia pale)

Yote hayo kwa ajili ya mapenzi ya kweli na urafiki wa dhati sana aliokuwa nao kwangu hakika niliumia na kufurahia kwa wakati mmoja.

  1. EDGAR
    Wanasemaga hakuna urafiki wa mwanamke na mwanaume bila kuwa na mahusiano ya kimapenzi nakataa kabisa

Huyu kaka alinipenda sana kama dada na mshkaji wake wa dhati mno

Halafu nikikumbuka sababu ya kujuana nae mpaka leo huwa nacheka tu

Edgar alikuwa dokta, kijana smart na mchapakazi sana

Nakumbuka aliwahi kuniambia “Mwajuma hii Dunia imesha kukataa, so pambana kwa vyovyote vile utobe”

Unajua kwanini aliniambiaga vile.. Ni sababu ya changamoto nilizowahi kupitia kwenye maisha yangu

Edgar alikiri kabisa yeye hajawahi pitia maisha kama yangu na kama angepitiaga basi asingeishi!

So alikuwa bonge la mshkaji sana aise na siri zangu nyingi alikuwa nazo yeye (hata Maria na Gwamaka hawajui vitu vyangu ambavyo Edgar anajua)

Edgar alitaka kunipa nyumba yao ya urithi nikae bure wakati najitafuta (hii nyumba ilikuwa chamazi mpya Ila haijaisha baadhi ya vitu) baba yake aliijenga mwaka mmoja kabla ya kufa kwake so ilikuwa mpya kabisa

Ila sikuweza kukaa kule sababu ya umbali na ilipo kuwa kazi yangu (kazi nilikuwa nafanyia banana ukonga pale AVIATION) wakati nimekosa mkopo wa chuo.

Huo niliona ni zaidi ya upendo wa Edgar kwangu, mtu ambae tulijua mjini na tukaamininiana sanaa.

So urafiki wa kweli siku zote kwanza hauna mipaka ya mapenzi

Urafiki wa kweli huja wenyewe automatic

Urafiki wa dhati hautaki sababu za msingi za kupendana

Urafiki wa kweli siku zote upo natural tu huja bila kutumia nguvu

Na urafiki wa kweli haunaga kipimo wala mashaka ndani yake

Ukiona una rafiki Ila kuna namna unahisi mapungufu ya urafiki wenu tambua kuwa haupo kwenye urafiki sahihi.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Simama Na Hatma Yako, Kwakuwa Hata Waliofanikiwa Waliamua Kusimama Na Hatma zao

Next Post

Hivyo Unavyojihisi Ni Sawa Ila Pia Unapaswa Kuendelea

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.