
Binaadamu hawana shukurani wala kumbukumbu kwenye mema na mazuri , usijimalize sana
Katika viumbe hai ambayo hupoteza uwezo wa kukumbuka mema haraka ni binaadamu
Binaadamu hata umpe roho yako, kuna siku atasahau kila kitu
Hakuna binaadamu mwenye uwezo wa kutunza mema milele
Wala hakuna binaadamu ambae hukumbuka mema aliyotendewa kwa namna ya uzito ule ule
Kosa moja tu hufuta kumbukumbu zote nzuri ulizompa
Ukitaka kukumbukwa milele tenda mabaya na maovu Ila kama unataka kusaidia pekee bila kukumbukwa basi tenda mema kisha nenda zako
Watu ni wepesi wa kukumbuka mabaya haraka mno na wazito wa kukumbuka mema
Hivyo kama unatoa kitu iwe kikubwa au kidogo kwa lengo la kulipwa mazuri zaidi mbeleni ndugu yangu unapoteza nguvu zako
Toa kwa nia njema kisha sahau kabisa, kama utakumbukwa sawa na kama ukisahaulika pia sawa
Ila tambua binaadamu yoyote uwezo wa kukumbuka mazuri ni mdogo sanaaaaa
Tenda mema 2000 kisha kosea 1 tu vidole vyote vitakugeukia
Mpe mazuri 100 sahau 1 tu basi mazuri yote yatafutwa haraka
Lakini pia akipata anapopewa zaidi ya unavyompa hapo ndio msaada wako hugeuka kama debe moja la maji baharini
Hivyo Basi usijamalize sana kisa watu haijalishi uhusiano wako na wao
Usijisahau kujipa furaha na kutumia vyako kisa shida za watu
Usiweke roho yako rehani kisa kusaidia sana watu
Na ikitokea umesaidia fanya kama umeangusha au umepoteza tu
Kamwe usitunze kumbukumbu na kutaka kulipwa sawa na ulichotoa.