Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Chagua Changamoto Zako

chagua changamoto zako
Photo by Tima Miroshnichenko on Pexels.com

Maisha ni safari ndefu yenye kila aina ya majaribu, mitihani na changamoto

Kila jambo kwa namna yake lina changamoto zake

Hakuna kitu ambacho kitakufanya kwa asilimia miamoja uwe salama bila misukosuko kadhaa!

Kila utakacho kichagua lazima ukubali changamoto zake yani ni kama unavyopenda boga basi utapaswa kupenda na Ua lake

Kwahio chagua changamoto Chanya zinazokukuza na kubadili maisha yako huku zikukupa nuru ya kesho yako

Usikubali kukumbatia changamoto zinazokuumiza na kukupa mateso huku zinashusha thamani na maana ya maisha yako

Songa mbele ukiwa umebeba changamoto zinazokufanya uone maisha kwa tafsiri ya maana na kusudi la kuumbwa kwako

Usikubali kuwa mtumwa kwenye maisha ya watu wengine

Usikubali kutumika kwa faida za watu wengine

Usikubali kulia na kuona Dunia kama sehemu ya maumivu

Tumeletwa Dunia kufurahia kwa kila sekunde inayopita

Chagua changamoto zako hata zikikutesa bado siku moja upate ujasiri wa kusimama kwa ushindi na kusimulia wengine funzo Chanya.

#YOU CAN WIN IF YOU WANT

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Tafuta Upekee Wako

Next Post

Hata Mbuyu Ulianza Kama Mchicha

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Usiogope Kujaribu

Usiogope kujaribu jambo hata kama unahisi huliwezi au ni gumu sana Kataa kabisa neno haiwezekani kwenye akili…

Tengeneza Mabawa Yako

Usikubali mazingira yakwamishe ndoto zako wala kukupa vikwazo vya kuwa unavyojiona kwa ndani Usikubali watu…