Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Changamoto Hukomaza Akili Na Mwili

Hizo changamoto zote unazopitia wala usihesabu kama mateso

Shida na mitihani uliyo nayo wala usichukulie kama kuteseka

Mazito na mapito yanayo kuandama wala usijione kama una teseka

Elewa kuwa hayo yote yanakupa ukomavu wa akili na mwili wako

Uzoefu wa hayo unayo pitia leo kuna siku utasema ningejua ningepitia mengi zaidi

Ipo siku utajipongeza kwa maisha ya sasa au zamani uliyo pitia

Kuna muda utafika utasahau hata maumivu yalifafanaje

Lakini utabaki na mafunzo ambayo kamwe hayato kuyumbisha kabisa tena

Hata dhahabu ili inga’e hupitishwa kwenye moto mkali sana

Hivyo jione kama dhahabu ya baadae

Jione mshindi wa baadae na hata jasiri wa baadae

Ujasiri unao jengewa kwa sasa huwezi kuuelewa mpaka muda ukifika

Kama unaona kupata hasara ya laki moja ni sawa na kupoteza kila kitu! Utaweza kuvumilia maumivu ya kupoteza milioni 10?

Kama unapata maumivu yasiyo isha kisa kuachwa na mwanaume kwa sasa ukiwa huna hata mtoto! Utaweza maumivu ya kuachwa na watoto 3?

Ikiwa unaumia kukosa kazi kwa sasa na huna familia! Utaweza kuhimili heka heka za kukosa kazi ukiwa na familia inayo kutegemea!?

Kumbuka yote ya sasa yanakuandaa kwa wakati ujao ambao unaweza kupitia au usipitie kabisa

Jambo la msingi ni kuwa imara kama vitani, hata kama hujui muda wa kuvamiwa lazima uwe na silaha zote!

Ujasiri wa maisha unafundishwa kupitia mchakato wa uzoefu wa changamoto za kila siku

Zipokee changamoto zako na zitatue wewe mwenyewe kwa niaba ya kesho yako.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Usiombe Samaki, Omba Kufundishwa Kuvua Samaki

Next Post

Sio Kila Mzee Anafaa Kuombwa Ushauri, Hata Wajinga Huzeeka

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.