Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Chunga Njia Unazopita Sasa Kusaka Mafanikio, Zisiwe Na Mwiba Kwenye Maisha Yako Ya Baadae

Maisha unayoishi sasa kuna siku utafurahia sana au utajutia sana

Haijalishi utakuwa na mafanikio makubwa zaidi au madogo sana

Majuto au furaha hutegemea na aina ya mtindo wa maisha ambao umechagua kuutumia kupata kipato chako!

Kutokana na sababu au kiu ya mafanikio unayotaka, kuna wakati unaweza kufanya kitu chochote kile

Hutozingatia vigezo, kesho yako, sheria za Dini wala za nchi au hata maumivu unayo sababisha kwa wengine..

Vile vile hutofikiria madhara na sintofahamu za maisha ya baadae kwakua maisha huwa hayagandi na kuna siku utajikuta kwenye maisha tofauti kabisa na hayo ya sasa

Hutowaza familia au vizazi vyako vijavyo au hata jamii kwa ujumla wake

Hutowaza maumivu utakayopata baada ya akili zako kurudi na shida zako kuisha au hata zisipoisha kabisa

Kitu pekee ambacho utakuwa nacho moyoni ni kiu ya mafanikio (haijalishi unataka mafanikio eneo gani).

Aina ya watu wanao kuzunguka sasa wanaweza kukufanya upite njia yoyote ile ili tu ufanikiwe

Njaa inayokusumbua sasa inaweza kukufanya uuze utu wako kwa gharama yoyote ili tu ujaze tumbo

Tamaa ulizonazo sasa zinaweza kukufanya ufuate mkumbo wowote kwa lengo la kupata unachotaka tu

ILA

Kuna muda utafika inawezekana ukawa kweli umepata mafanikio uliyo taka au hujafanikiwa kabisa,

Kumbukumbu za matukio mabaya zitakusonga kwenye akili yako kila sekunde

Utakumbuka kila baya ulilofanya kwa sababu za kiu ya mafanikio yako

Utahisi hali ya kujuta kupitiliza haijalishi mafanikio hayo umepata au hujapata

Utatamani upotee uende mbali sana kwa maumivu na majuto ya mambo uliyofanya haijalishi yalikuwa ya siri au dhahiri kwa watu

Lazima utalipa kwa kiwango kile kile, mateso na mchakato mbaya uliopita nyuma!

Sio lazima ulipe kwa wengine waliodhurika kupitia wewe la hasha!

Malipo utayapata wewe binafsi ndani yako mwenyewe kwenye moyo na roho yako!

Na hapo utagundua kuwa mafanikio hayana maana yoyote zaidi ya kutengeza historia ya maisha yako iliyo na maana kwako binafsi, jamii na Mungu wako

Bila kusahau mafanikio yanayo ambatana na amani au furaha ya dhati ukiondoa pesa, nyumba au hata magari ya kifahari.

ANZA SASA KUBADILI NJIA ZAKO HUJACHELEWA.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Maisha Sio Mashindano, Shindana Na Jana Yako

Next Post

Kuna Kumbukumbu Za Maisha Hazina Ufutio, Chunga Tamaa Zako

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Usiogope Kujaribu

Usiogope kujaribu jambo hata kama unahisi huliwezi au ni gumu sana Kataa kabisa neno haiwezekani kwenye akili…

Huruhusiwi ku copy makala hii.