Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Dunia Ina Mambo Mengi Sana, Chagua Yako Machache

Hapa Duniani kuna mambo ya kila aina kwa kila namna

Licha ya ukubwa wa Dunia, mabara na nchi zake

Kuna watu wengi sana ambao kila mmoja kwa namna yake ana kitu tofauti na mwingine!

Kuanzia tabia, akili, mawazo na hata muonekano

Kuna mambo hufanyika kwa watu fulani ambayo ni kituko kwa wengine

Kuna yale mazuri sana kwa watu fulani lakini huonekana ya ajabu mno kwa wengine

Kuna tabia mbaya sana tena zenye kuchukiza mno kwa watu aina fulani, Ila ni nzuri mno na zinazo heshimika kwa watu wengine

Pia kuna mila na tamaduni za ajabu sana kwa mataifa fulani, Ila zinapendwa kwa mataifa mengine!

Usisahu biashara na kazi mbalimbali za watu aina mbalimbali

Kuna biashara nzuri sana na zenye faida kwa mtu fulani Ila mbaya zaidi kwa mwingine

Kuna kazi nzuri kwa mtu yule Ila kazi ile ile ikawa mbaya sana kwa mtu mwingine,

Kipato kidogo kwa mtu huyu kinaweza kuwa ndio utajiri wa mwingine!

Hivyo kamwe huwezi miliki na kufurahia kila kitu sawa na wengine!

Huwezi elewa maisha ya kila mtu kamwe

Wala huwezi lazimisha mambo yawe sawa kwa kila mtu

Hivyo unapaswa kuchagua vichache vyenye maana kwako,

Kisha vishikilie kwa mikono miwili na ishi ndani yake

Halafu vingine vyote vifanye kama sehemu ya utalii wa macho na masikio yako!

Yani ukiviona au kuvisikia basi viache hapo hapo na zingatia yako

Tofauti na hapo utachangayikiwa na kupoteza muelekeo kabisa

Utaweka roho juu na kuona Dunia kama sehemu mbaya isiyofaa au ipo kwa ajili ya wengine tu

Utakosa muelekeo wa nini ushike au nini uache, kipi uamini na kipi uache

Kwa sababu ya kutaka mambo yote hata yasiyo kuhusu au kuwa na faida kwako

Zingatia maisha yako, tafuta maana ya maisha yako na ishi kwenye njia zako

Kiufupi ya Ngoswe muachie Ngoswe

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Kama Ndoa Haikupi Heshima Wala Nafasi Ya Kupigania Malengo Yako, Hio Haifai Kuwa Ndoa

Next Post

Hujaumbwa Kuteseka, Mateso Unajisababishia Wewe Mwenyewe

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.