Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Hata Mbuyu Ulianza Kama Mchicha

hata mbuyu ulianza kama mchicha
Photo by Sergey Guk on Pexels.com

Huo Mbuyu mkubwa sana, unaokutisha kila ukipita chini yake kwa ukubwa, urefu na Uimara wake kuanzia mizizi, shina mpaka matawi

Kumbuka nao pia ulianza kama mbegu ndogo ya mchicha!

Ukakuwa taratibu kwa kujenga himaya yake chini kwa chini kwanza

Mbuyu ulianza kutengeneza mizizi imara ndani ya ardhi kabla ya kupanda kujenga himaya kubwa kwa juu ya ardhi,

Kama mbuyu usingejenga mizizi imara na migumu pia isingiwezekana kuwa mkubwa sana kwa juu

Hakuna anaejua mangapi yalifanyika ndani ya ardhi kabla ya kuonekana mkubwa sana kwa juu mbele ya macho ya kila anae utazama!

Hivyo Basi usiogope kuanzia chini, usikate tamaa kutengeneza himaya yako, usijione mnyonge kwa kuanza na kidogo

Kumbuka wakati unaanzia chini ndio wakati unatengeneza himaya yako na misingi imara kwa ndani kabla hujaweka himaya kwa nje.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Chagua Changamoto Zako

Next Post

Tengeneza Mabawa Yako

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Tafuta Upekee Wako

Usikubali kuwa wa kawaida wala kufanya mambo wanayofanya wengine na yaliyozoeleka Mafanikio huja kwa kufanya…