Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Kubali Uhalisia Kuna Mambo Hayabadilishiki

Kuna vitu huwa havibadiliki haijalishi utatumia nguvu kiasi gani

Kuna mambo yakishatokea huwa yametokea

Kuna maamuzi yakishapitishwa huwa yamepitishwa

Na kuna watu wakishabadilika huwa wamebadilika

Sasa kuendelea kutaka mambo yawe tofauti kwa namna unayotaka wewe ni moja kati ya njia kuu ya kujiumiza wewe mwenyewe

Kuna muda njia pekee ya kupata nafuu ni kukubali UHALISIA

Usilazimishe nyekundu kuwa kijani mahala ambapo haiwezekani

Kukubali matokeo au uhalisia ni nusu ya kupata dawa na tiba

Acha kabisa kulazimisha mambo ambayo yameshindikana

Utamaliza pesa na muda wako bure mbaya zaidi utakosa raha na amani ya maisha

Kama jambo haliondoi uhai wako wala afya yako… Kubali uhalisia wake tu

Afya na uhai pekee ndio hazina kubwa zaidi ya maisha

Vitu vilivyobaki vyote vinaweza kupatikana wakati wowote

Haijalishi itachukua muda kiasi gani kuvipata tena!

Vile vile bila kujali ukubwa wa maumivu unayopitia au gharama ulizotumia.. Kubali Uhalisia

Pokea matokeo kwa mikono miwili kisha jiruhusu na jipe nafasi ya kupata vilivyo bora zaidi

Kila jambo hutokea kwa sababu maalumu kwenye maisha

Kwahio jifunze kutotaka mashindano yasiyo na msingi hata kwenye vitu vinavyotafutwa na kupatikana

Kubali Uhalisia wa mambo na utapata nafasi na fursa mpya pengine nzuri kuliko za mwanzo.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Usisahau Kuishi Wakati Unatafuta Maisha

Next Post

Binaadamu Husahau Mema Haraka, Usijimalize Sana

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Usiogope Kujaribu

Usiogope kujaribu jambo hata kama unahisi huliwezi au ni gumu sana Kataa kabisa neno haiwezekani kwenye akili…

Huruhusiwi ku copy makala hii.