Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Kufa Na Tai Shingoni Kwenye Baadhi Ya Shida Zako

Haipendezi kila wakati kulilia shida zako kwa watu

Sio busara kila saa kutangaza matatizo unayopitia

Wala sio kitu chema sana kuzungumza changamoto zako kwa kila mtu

Elewa kuwa kila mmoja ana shida zake binafsi

Kulia lia shida kila saa hukera watu, unajidhalilisha binafsi na unaondoa uhusiano mzuri baina yako na wengine

Hakuna ambae hana uhitaji wa kitu fulani au msaada fulani

Ila huamua kufa na TAI shingoni mwao kwakua huelewa hata wengine wana shida zao pia

Kuna mtu ukikuta analalamika kuwa hajasaidiwa na ndugu au rafiki zake,

Unaweza hisi aliwekeza huo msaada kwao hao watu kwa lengo la kurudishiwa siku atakapo hitaji!

Yani mtu mwingine ni mkubwa sana kiumri, Ila ukisikiliza maongezi yake utachoka kabisa

Kila saa ni shida hii, mara shida ile, mara malalamiko Haya mara malalamiko yale

Hana muda wa kuongea mambo mazuri yanayo leta furaha

Hana muda wa kusambaza nguvu chanya kwa wanao mzunguka

Zaidi ya malalamiko na vilio vya shida, hakuna kipya unaweza jifunza kutoka kwake!

Hali ya kupenda kusaidiwa kila wakati ndio hufanya akili kukosa uchanganuzi wa matatizo

Ndio imefanya wadada kudanga na wakaka kubadili utu wao

Hufanya akili kulala usingizi mzito na kutowaza chochote

Zaidi ya msaada na kitonga au mterezo kutoka kwa wengine kama ganda la ndizi,

Hupelekea tatizo linapotokea tu, akili hukimbilia kutafuta mtu wa kusaidia!

Na hii ndio imefanya hata viongozi wetu wakubwa wa nchi kutwa kutembeza mabakuli ya kuomba msaada

Licha ya wingi wa Rasilimali zilizopo, akili zao zinashindwa kabisa kuchanganua namna ya kuleta maendeleo kwa kutumia utajiri wa asili tulionao

Ila haraka hupata mbinu na mikakati ya kuomba misaada na mikopo nchi za wengine

Taifa haliwezi kujikwamua kupitia misaada haijalishi msaada wa mtu mmoja mmoja au nchi nzima

Tunapaswa kutumia akili zetu kuleta mapinduzi kwanza maeneo mbalimbali

Kisha msaada huombwa pale ambapo inalazimika Kuombwa na sio kwenye kila kitu

Hakuna jambo baya kama kujiona muhitaji wa kusaidiwa kuliko wengine

Kujiona dhaifu na kutaka kuonewa huruma kutoka kwa wengine

Hakika hii ni moja kati ya vitu ambayo mimi binafsi huninyima usingizi

Na hata kukosa hamu ya kula kabisa napokutana na mtu mzima anaomba msaada au analalamika eti hasaidiwi!

Badilisha namna unavyo fikiria, ongeza uwezo wa kutatua matatizo yako bila kuhitaji msaada wa wengine.

KUFA NA TAI SHINGONI KWENYE BAADHI YA SHIDA ZAKO

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Kisasi Kizuri Zaidi Ni Kuwa Bora Zaidi Ya Mwanzo

Next Post

Kuwa Na Afya Ya Akili Nzuri Ni Muhimu Sana Kuliko Mafanikio Ya Fedha

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.