
Kulinda afya ya akili binafsi ni kitu muhimu sana kwenye maisha
Asilimia kubwa sana ya maisha tunayo ishi hususani nchini Tanzania ni chanzo kikubwa cha afya ya akili Kutokuwa sawa
Watu wengi wanapitia changamoto ngumu bila wao kujua
Aina ya maisha na mazingira kwa asilimia kubwa Tanzania ni magumu sana kiasi kwamba hufanya akili kuvurugika mara kwa mara
Watu wamejaa visirani na makasiriko ya hapa na pale
Kila mmoja anaishi kwa machale muda wote bila kujiamini
Ugumu wa maisha na matatizo ya kila aina pia ni chanzo cha akili kweda resii sana
Hata upatikanaji wa huduma mbali mbali ni katika namna ngumu inayopelekea akili za watu wengi kukosa utulivu
Kwa hakika ili akili ipate wakati mzuri wa kufikiri na kugundua mambo mengi, utulivu ni jambo la msingi zaidi
Wengi wanaishi maisha magumu sana ukiachilia ugumu wa kipato, bila wao wenyewe kujua
Tanzania hata ujitahidi kwa kiwango gani kuweka akili sawa bado kuna namna utashindwa,
Kutokana na mtindo wa maisha ya watu kila siku
Vile vile mtindo wa maisha ulio andaliwa na viongozi wanaoshikilia nchi
Hakika watu wanateseka sana hata bila wao kujua kama wanapitia mateso
Kila kitu kupata ni shida na mlolongo mrefu sana licha yakuwa haki kwa mtu
Kuna watu wengi sana wakubwa kiumri hata ki cheo na mafanikio Ila mambo wanayofanya ni kama watoto wadogo!
Matendo na maneno yao hayaendani kabisa na umri au cheo katika jamii zao
Hakika ni msiba mzito sana kwa wakazi wa nchi yetu kwa ujumla
Hii ndio zaidi inapelekea mmomonyoko wa maadili kuzidi kukithiri maana hata hao waliopewa dhamana ya kuweka sawa maadili wanaona sawa tu kwasababu na wao afya zao za akili zinaona sawa
Kila mmoja ana pambana kuziba njaa ya tumbo lake bila kujali mangapi yana haribika!
Njia kubwa zaidi ya kusaidia kuishi na kuweka akili sawa ni pamoja na kuchukulia kila kitu katika namna chanya
Kutofatilia kila jambo linalotokea hasa kama ni nje ya malengo yako
Bila kusahau kujiweka mbali na mazingira au mtu yoyote ambae ni sababu ya kuharibu akili yako
Kufanya tahajudi mara kwa mara na kutafuta muda wa peke yako
Kufuatilia vitu vichache vinavyojenga na kuboresha uwezo wa kufikiri
Bila kusahau kusoma sana vitabu na kusikiliza podcast mara kwa kwa mara