Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Kwenye Maisha, Hakuna Anae Wahi Wala Kuchelewa, Kila Mmoja Hupata Kwa Muda Sahihi

Usiumizwe sana na wanao tangulia kupata kabla yako

Usipate presha kuona wengine wametangulia zaidi yako

Usilie sana kuona wengine wanapiga hatua za mafanikio kuliko wewe

Usijidharau au kujiona mnyonge sababu ya wengine wanaokuzidi kwenye maisha

Usikimbizane na wengine kwa kuhisi unaachwa nyuma zaidi

Usimlaumu Mungu na kudhani anakuacha kwa makusudi

Usifanye mambo mabaya na maovu kisa haraka ya kutaka kuwa kama wengine

Usikimbilie mahala ambapo maisha bado hayaja kupeleka

Kuwa na subra, Hakika kila mmoja hupata kwa muda wake sahihi

Hakuna anae wahi sana wala anaechelewa sana hapa Duniani

Hakuna mjanja sana wala mjinga sana kwenye muda wa kufanikiwa

Kupata mapema sio tiketi ya kudumu nacho milele

Wapo waliotangulia kupata na sasa hawana tena

Na wapo waliochelewa kupata na bado wanavimiliki

Ikiwa unafanya unayopaswa kufanya katika njia zako

Unajituma na kupambania hatma ya maisha yako

Unatafuta fursa kwa nguvu na akili zako

Unafanya juu chini kuboresha maisha na kutimiza malengo yako

Basi inatosha sana na huna haja ya kuumia kwa sababu ya wengine walio mbele yako

Heshimu sana mapambano yako na kuna siku utapata kwa muda na wakati sahihi.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Jifunze Kunywa Mchuzi Wa Mbwa Ukiwa Bado Wa Moto

Next Post

Umeumbwa Kuitawala Na Kutumikiwa Na Dunia

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.