Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Maisha Sio Kombolela Ila Kuna Watu Wanabutua

Wakati unasema hakuna mapenzi ya kweli, kuna watu wanafunga ndoa kila siku

Wakati unasema biashara ngumu, kuna watu wana fungua biashara mpya kila siku

Wakati unasema hakuna ajira, kuna watu wanaajiriwa kila siku! Na kuna kampuni zinatangaza kazi kila kukicha

Wakati una fikiria kuhama nchi au mkoa fulani kuna watu wanapigania kuhamia ulipo kila siku kwa uwepo wa fursa ambazo wewe hujaziona!

Wakati unasema utaanza kesho, kuna wenzako wanakesha kufanya kitu hiko hiko kila siku!

Wakati unasema maisha magumu, kuna wale wanaokesha wakitumia pesa kila siku!

Kila unaposema ukiwa na kitu fulani ndio utafurahi kuna watu hawana chochote na wana furaha ya kweli ndani yao

Kila unaposema biashara fulani hailipi kuna watu wanafanya biashara hio hio miaka kibao na wanaendesha maisha yao.

Kimsingi hakuna kitu kibaya, kigumu wala kisichowezekana

Yote hutegemea upande wako wa akili ulipoelekea

Ukiamua kuona ugumu Hakika itakuwa zaidi ya ugumu na ukiamua kuona wepesi bila shaka utapata njia ya kufanya unachotaka…

Maisha sio kombolela japo wapo wanao butua..

Maisha sio bahati Ila wapo wanao bahatisha..

Maisha sio mateso lakini wapo wanao teseka!

Maisha ni uchaguzi wa matumizi ya akili kwa mtu binafsi,

Kila mmoja hufanya maamuzi yeye mwenyewe ya kuitawala akili yake na akili huamua kumzawadia kile kinachomfaa.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Anza Kujisamehe Wewe Mwenyewe Kabla Hujasamehe Wengine

Next Post

Muda Hauto Simama Ukigoma Kwenda Nao

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next