Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Sio Kila Mlango Uliofungwa Pia Umelokiwa

Sio kila mlango unao uona mbele yako kwa macho ya nje umefungwa basi pia umelokiwa kwa funguo!

Kuna Milango imeegeshwa tu lakini kitasa kipo wazi

Kuna Milango ina vitasa vibovu kabisa au hata upo kwenye marekebisho

Kuna Milango imesahulika kufungwa na wahusika kwa bahati mbaya

Kuna Milango haifungwagi kabisa kwa funguo kutokana na sababu mbali mbali

Kuna Milango asili yake migumu tu mpaka utumie nguvu kufungua lakini haina loki yoyote

Ipo milango inatumia funguo Sawa na funguo uliyonayo wewe mwenyewe

Kuna ile Milango imejifunga sababu ya upepo tu lakini haina loki yoyote

Hivyo kabla hujasema huwezi kuingia ndani … Shika kitasa kwanza

Shika kitasa kwa nguvu na tumia uwezo wako wote kusukuma mlango ulio mbele yako…

Kama hautofunguka angalau unaweza kuwa na sababu ya kusema umeshindwa kuingia ndani!

Hivyo hata kwenye maisha yako kuna fursa zinakupita kutokana na mtazamo wa nje tu,

Kumbe ndani ya fursa hio kila kitu kipo wazi kina kungoja wewe!

Badili mtazamo wako… Utabadili maisha yako.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Zingatia Alama Zako Za Nyakati Ili Ufanikiwe

Next Post

Anza Kujisamehe Wewe Mwenyewe Kabla Hujasamehe Wengine

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Usiogope Kujaribu

Usiogope kujaribu jambo hata kama unahisi huliwezi au ni gumu sana Kataa kabisa neno haiwezekani kwenye akili…

Tafuta Upekee Wako

Usikubali kuwa wa kawaida wala kufanya mambo wanayofanya wengine na yaliyozoeleka Mafanikio huja kwa kufanya…