Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Tumia Mshahara Na Kipato Chako Binafsi Kusapoti Biashara Yako Mpaka Pale Biashara Yako Itakapoweza Kusapoti Kipato Na Maisha Yako

Huwa napata kigugumizi sana napoona mtu yupo tayari kutumia pesa za biashara yake kufanya matumizi binafsi lakini kamwe hawezi tumia pesa zake binafsi kukuza biashara yake!

Siku zote lazima ukubali kuumia biashara yako, kabla biashara haijaanza kukuhumia wewe!

Kama una kazi na kipato nje ya biashara unayofanya basi unapaswa kuwekeza kwenye biashara yako wakati bado changa

Kama ambavyo unajihudumia wewe binafsi kwa kipato chako binafsi, ndivyo unapaswa kuhudumia biashara yako!

Njia rahisi zaidi ni kubadili aina ya vipaombele binafsi na kuacha baadhi ya matumizi mengine kisha kuelekeza pesa kwenye biashara kwanza kwa muda maalumu

Biashara inataka matunzo ili iweze kukua na kustawi

Biashara inataka uwekezaji ili iweze kukulipa zaidi

Biashara inataka heshima nayo pia itakuheshimu mbeleni.

Mtu pekee anaeweza kujua uchungu wa biashara yako, ni wewe mwenyewe

Mtu pekee anaeweza kutunza na kustawisha biashara yako, ni wewe mwenyewe!

Mtu pekee anaeweza kuokoa biashara yako, ni wewe mwenyewe.

Fanya ufanyavyo lakini hakikisha kuwa unaijali, kuthamini na kuwekeza kila ulichonacho kwenye biashara yako

Biashara ikitunzwa vyema, itanawili na ikinawili itavutia zaidi kisha itakulipa mbeleni

Gharama zote unazotoa leo hii mfukoni kwako kwa ajili ya biashara yako, kuna siku zitakulipa zaidi kupitia faida au uzoefu!

Usiogope kujitoa muhanga kwa lengo la kukuza biashara yako

Kwa sababu ikitokea umepata na kubutua utasahau kila shida, na ikitokea umekwama utajifunza pakubwa, jambo la msingi ni hutotoka patupu!

Tumia sehemu ya mshahara wako weka kwenye mahitaji muhimu na mapungufu ya biashara yako mara kwa mara mpaka pale biashara itaanza kujiendesha yenyewe

Biashara ikianza kujiendesha ndio utaona malipo yake rasmi

Kwani gharama zako zote zitarudi na itasapoti maisha na kipato chako.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Maneno Hayarudishiki Mdomoni, Chunga Sana Ulimi Wako

Next Post

Kama Huwezi Kuchagua, Kubali Kula Wa Chuya

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.