Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Umeumbwa Kuitawala Na Kutumikiwa Na Dunia

Hakuna aliyeletwa Duniani kwa ajili ya kuteseka

Kabla Mungu hajamuumba Binaadamu aliumba Dunia na vilivyomo

Kwa sababu moja tu Binaadamu anapaswa kutawala vitu, sio kutawaliwa

Dunia yote pamoja na vilivyomo, vimeumbwa kwa ajili ya watu (viumbe hai)

Kila kinachofikika kipo kwa ajili ya kutumikia watu

Mazingira yote unayoona na vilivyomo ndani yake, vipo kwa ajili yako wewe pia

Vitawale na tawala Dunia yako

Binaadamu yupo kwa ajili ya kutumikiwa na vitu, sio Kutumikia au kutumika

Ukiona unatumika sana kwa ajili ya maisha ya Dunia elewa kuwa kuna kitu unakosea!

Ukiona unaumizwa sana kwa ajili ya maisha ya Dunia basi tatizo lipo kwako mwenyewe!

Ukiona unakosa raha kwa ajili ya jambo lolote lile kwenye maisha, basi wewe ndio changamoto yenyewe!

Na chanzo kikubwa zaidi cha kufanya maisha yakupeleshe na kukutumikisha, ni kuishi nje ya mstari wako!

Kuishi nje ya mstari wako kabla ya kuchora ramani sahihi ya mstari mwingine!

Kwa sababu ya tamaa na haraka ya maisha ambayo hujaweka utaratibu maalumu wa kufika unapotaka

Kila mmoja ana mstari wake wa maisha na ukomo wa kutumikiwa na Dunia yake

Dunia haitumikii kila mtu kwa namna anayotaka bali kwa kanuni maalumu ya mstari wa kwenye maisha ya mtu husika

Mstari huo husogea taratibu na kumpa nafasi mtu kuishi maisha anayopaswa kuishi kulingana na nyakati sahihi

Nyakati ambazo huambatana na kiwango cha mafanikio yake

Kama utaishi ndani ya mstari wako hakika lazima ufurahie Dunia maana ndio utaratibu unaopaswa kufuatwa!

Maisha yana kanuni zake ukiondoa kanuni zako wewe ulizojiwekea

Na pia ukiona unapitia mateso mengi sana na Dunia inakuwa chungu sana, basi ukweli ni kuwa chanzo ni wewe umevuka mstari kabla ya muda sahihi

Rudi nyuma kwenye mstari wako kwanza kabla mambo hayajawa magumu zaidi

Hakina utaona utamu na ladha ya maisha yako.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Kwenye Maisha, Hakuna Anae Wahi Wala Kuchelewa, Kila Mmoja Hupata Kwa Muda Sahihi

Next Post

Kama Huwezi Kujenga, Basi Angalau Usibomoe

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Tafuta Upekee Wako

Usikubali kuwa wa kawaida wala kufanya mambo wanayofanya wengine na yaliyozoeleka Mafanikio huja kwa kufanya…

Huruhusiwi ku copy makala hii.