Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Unapo Nyoosha Kidole Kimoja Kwa Mwingine, Kagua Uelekeo Wa Vidole Vilivyobaki

Umewahi kujiuliza kwanini ukinyoosha kidole kimoja kwa mtu, basi vingine hukugeukia wewe?

Hivi unajua kuwa siku zote unapaswa kukagua madhaifu yako kabla ya kukagua madhaifu ya wenzako?

Kuna watu hujiona bora sana, kisha huhisi wengine kama vile hawana maana kama walivyo wao!

Hawa ndio wale ambao kutwa hupambana kutafuta makosa ya wenzao,

Hawa ndio wale ambao huonaga baya kwenye kila afanyacho mwingine

Hupenda kukosoa sana na kuhisi kama wengine hawajui kitu wala hawana akili nzuri

Hujaribu kukagua madhaifu sana badala ya kukagua mazuri ya mtu.

Asili ya maisha inatutaka kabla hatujaona makosa ya wengine basi tuanze kujikagua sisi kwanza

Kabla hujaona madhaifu ya mtu mwingine, anza kukagua madhaifu yako wewe binafsi kwanza

Kabla hujamsema mtu mwingine kwa mabaya basi anza kukagua mabaya yako kwanza.

Usiwe mwepesi sana kuona makosa ya wengine kabla hujaona makosa yako

Tambua kuwa Duniani watu hawafanani na kubwa zaidi watu hawajakamilika.

Hakuna mkamilifu kamwe na kila mmoja kuna namna tu hajatimia kwa asilimia zote kwenye eneo fulani

Hivyo ni vyema kuheshimu na kuhifadhi madhaifu ya wenzetu kwa namna ambayo tungependa madhaifu yetu yahifadhiwe pia.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Huhitaji Maombi Wala Mganga Kuondoa Roho Zinazo Kutesa, Unazo Nguvu Na Uwezo Wewe Mwenyewe

Next Post

Uzito Wa Hoja Hupimwa Kwa Hoja Nzito Zaidi Kwa Maana Hakuna Mzani Wa Hoja

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.