Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Usimsaidie Mtu Msaada Ulioficha Manyanyaso Kwa Ndani

Nilipokuwa na umri kati ya miaka 9 mpaka 15 mama alishindwa kunilea kutokana na ugumu wa maisha

Mbaya zaidi baba yangu nilimuona mara mbili tu katika kipindi cha uhai wake na hata sikumbuki sura yake tena.

Nililelewa na ndugu zangu upande wa baba yangu huko kigoma kasingirima

Babu alinichukua baada ya kuona mama hawezi kumudu gharama za kunilea kwa wakati ule

Hio ilikuwa baada ya mama kushindwa kuninunulia dawa za shillingi elfu 1000 tu kwa wakati ule na hali yangu ilikuwa mbaya kwa homa kali

Mara baada ya Babu yangu kufariki, maisha yalikuwa machungu sana

Mateso na manyanyaso mengi mno nilipitia kutoka kwa ndugu zangu wale

Kuna wakati shangazi yangu ALINIMWAGIA KOPO LA MATE YAKE (alikuwa mjamzito hivyo kutema mate kwenye kopo)

Fikiria mate ya usiku mzima aliyohifadhi kwenye kopo alinimwagia mimi asubuhi

Kosa likiwa kutopika chai kwa wakati kutokana na wingi wa kazi za pale nyumbani!

Mengi yalitokea magumu na mazito sana kiasi kila nikikumbuka huwa napata maumivu makali sana

Kupigwa ilikuwa kawaida mno na hata kutukanwa matusi mazito mno nilizoea

Kuna siku baba yangu mdogo aliwahi kunipiga fimbo nyingi sana huku akinikokota kama mwizi kuanzia chumbani mpaka nje ya uwanja

Nilikuwa kwenye siku zangu za kike, hakujali kabisa namna ambayo damu zilimwagika kila alivyo niburuza

Licha ya wingi wa watu waliozunguka nje kushuhudia navyopigwa na uwepo wa jinsia za kiume hakujali wala kuona huruma!

Kosa lilikuwa kulala mpaka saa 2 asubuhi kwakua nilisema naumwa sana tumbo la hedhi

Mbali na kufanya kazi nyingi sana za nyumbani, hakuna aliyejali wala kuona mazuri yangu

Licha ya kujituma na kujitoa kwa nguvu zangu zote hakuna aliye hesabu kabisa

Sikuwa binti pekee pale nyumbani, kulikuwa na mtoto wa babu umri sawa na wangu ambae nilimwita shangazi

Mama yake (bibi) yangu hakutaka mwanae afanye chochote kile na hata alipokosea hakuadhibiwa kabisa.

Lakini kwa nje walitangaza kuwa wananilea na kunisaidia maisha na masomo yangu!

Naweza kusema moja kati ya kumbukumbu zangu mbaya za utoto zilianzia pale kwenye ile nyumba

Japokuwa walikuwa ndugu zangu wa damu Ila walinitesa kama mtu baki

Na mpaka sasa kigoma ni moja kati ya mikoa ambayo hunipa kumbukumbu mbaya sana,

Kila napo fikiria kwenda hupata wakati mgumu mno hata kukaribia ile nyumba

Japokuwa ndio nyumbani na asili yangu ipo kule

Na hata ninapo amua kwenda kutembea siku zote huwa nafikia nyumba za kulala wageni!

Unaweza kumfanyia mtu mabaya kwa kisingizio kuwa una msaidia

Ukampa msaada kweli lakini msaada uliojaa maumivu

Yule mtu atavumilia sana kwakuwa anahitaji kujikwamua sio kwakua anafurahia unachofanya

Na siku akipata nafasi ya kutoka hapo kamwe hawezi kumbuka msaada wako kabisa

Unaweza kusema ulimlea mtoto Ila baadae amepata maisha yake na hakumbuki fadhila

Kumbe ulimpa fadhila mbaya zilizojaa maumivu makali mno

Kama umeshindwa kumlea au kumsaidia mtu bila manyanyaso ni bora muache aende kuliko kumjengea kumbukumbu mbaya kichwani kupitia msaada wako

Watu wengi sana hupitia mateso mengi kisa misaada wanayopewa

Baada ya muda huja kulipiza mabaya hata kwa vitendo kisha watu hutangaza kuwa alisaidiwa na kalipa ubaya

Kumbe wema aliopewa ulificha ubaya kwa ndani toka mwanzo kutoka kwa walomsaidia.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Kuwa Na Afya Ya Akili Nzuri Ni Muhimu Sana Kuliko Mafanikio Ya Fedha

Next Post

Kama Ndoa Haikupi Heshima Wala Nafasi Ya Kupigania Malengo Yako, Hio Haifai Kuwa Ndoa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.