Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Usiombe Samaki, Omba Kufundishwa Kuvua Samaki

Watu wengi sana kwa sasa imekuwa kawaida sana kuomba Msaada kwa wengine

Kitu ambacho sio jambo baya sana na wala sio jambo jema kabisaaa

Ubaya unakuja pale ambapo mtu huyu huyu anataka msaada wa muda mfupi

Lakini hataki hata kusikia kufundishwa kuingiza kama zile anazoingiza muombwaji

Yaani anataka umpe pesa au kitu cha thamani lakini hata mara moja hajawahi kuumuliza huyu huyo mtu nifanye nini niwe kama wewe

Hataki hata kusikia mchongo ulivyo wala mchakato unavyoenda Ila anataka apewe chochote kitu tu

Halafu akinyimwa anajenga chuki na ubaya kwa mtu tena bila aibu kabisa

Hujui magumu mangapi wenzako wanapitia kwenye utafutaji

Hujui kuna muda wanakesha na hata wanapata maneno makali kwa mabosi zao au wateja

Hujui hasara ngapi wanapata na hata maumivu kiasi gani wanayo

Huelewi kabisa hata wamepoteza pesa kiasi gani kwenye kupata hiko walicho nacho

Unachojua ni kuomba tu kirahisi kama vile ni chako wewe au umewekeza kwao

Halafu ukinyimwa unaanza kutangaza ubaya kwa mtu!

Mbaya zaidi ukiambiwa njoo na wewe ufanye hiki upate pesa unasema bila aibu kabisa eti hayo mambo yenu mimi siwezi!

Au sina muda kuna inshu nafanya… Ajabu izo inshu hazikupi chochote

Yani wewe una lala ndani wenzako wanakesha usiku na jua la mchana halafu kirahisi tu unaomba kuungiwa mazaga!

Hebu badilika siku moja na wewe useme chukua hii.. badala ya Naomba hii

Yani na wewe uwe unatoa kwanza ujue uchungu wa kutoa kitu.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Namna Ya kupata Hamasa

Next Post

Changamoto Hukomaza Akili Na Mwili

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Tengeneza Mabawa Yako

Usikubali mazingira yakwamishe ndoto zako wala kukupa vikwazo vya kuwa unavyojiona kwa ndani Usikubali watu…

Huruhusiwi ku copy makala hii.