Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Usiruhusu Hofu Ikukwamishe

Pinga hali ya kuogopa na ikatae kwa nguvu zotee

Kataa hali ya kusita kufanya jambo kwa uwezo wako wote

Usiruhusu akili yako ikuoneshe vikwazo na changamoto badala ya maarifa yakinifu

Pinga kabisa kubaki nyuma, kujishtukia na kujiona dhaifu

Duniani tunaishi mara moja kwahio tumia muda wako vyema

Hakuna ugonjwa wa hofu wala aibu bali wewe mwenyewe Ndio umechagua kubaki salama ukiogopa kuchekwa endapo utashindwa kwenye kitu fulani

Kushindwa ni kawaida wala wewe sio wa kwanza, ni bora ujaribu ushindwe uchekwe kuliko kufurahisha watu kisha kuchekwa utakapokuwa omba omba

Watu wanaokucheka leo, watakucheka hata kesho kwakuwa utakuwa umechagua kuona upande wa vicheko vyao

Vaa miwani nyeusi, jifanye kipofu na weka ujasiri kisha anza kufanya hicho kinacho kugopesha.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Tumia Nafasi Uliyonayo Kikamilifu

Next Post

Mbinu Za Kupata wateja

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Kula Kondoo Aliyenona

Kama umeamua kula kondooo kula aliyenona haswaaa, Kiasi kwamba hutojutia kabisa hata kama alikuwa kondoo wa wizi…