Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Wakati Mwingine Muombe Mungu Ujasiri Na Roho Ngumu Pekee

Mungu ana wahitaji wengi sana wanaotaka msaada wake

Kila muhitaji ana sababu za msingi kuliko mwingine!

Kuna wahitaji wana maradhi ya muda mrefu

Kuna wengine walemavu wa kudumu

Kuna wale toka wazaliwe hawajawahi kupona kabisa

Kuna ambao walipata matatizo ya kusababishiwa na hawana kosa lolote

Wapo ambao ukiwasikiliza utaishia kulia kuliko wao wanavyolia!

Kuna watu toka wamezaliwa hawajawahi kuonja ladha ya furaha wala raha

Halafu kuna wale njaa kwao ni kama mseto tu, hata wakipata shibe tumbo linashtuka!

Na wengine kibao ambao wana matatizo na changamoto za kila aina ngumu sana na nzito mno za kiuumbwaji.

Sasa hawa wote kila sekunde huomba msaada kwa Mungu kila mmoja kwa namna yake

Unahisi Mungu anapaswa kumsaidia nani kati yao na wewe?

Chunguza shida zako halafu linganisha hata na shida za wachache wahitaji kuliko wewe unao wajua…

Ndio utagundua kuwa hupaswi kuomba wala kulilia msaada wowote kwa Mungu zaidi ya kupambana na changamoto zako

Hata kama Mungu atakupa unachotaka muda huu, baada ya siku chache utaomba kingine!

Binaadamu hajawahi kuridhika ukizingatia changamoto haziwezi kuisha kamwe!

Kila utakachomiliki au kupewa kina changamoto zake..

Ukiwa mtu unaetaka msaada wa Mungu kwa kila changamoto, utaishia kukosa raha na kukufuru kila siku!

Badala ya kuomba msaada wa kitu fulani kwa Mungu, muombe akupe ujasiri kwa kila changamoto na matatizo unayo kutana nayo

Akupe nguvu na ujasiri wa kupambana na kila mtihani utakaokuja mbele yako

Akupe roho ngumu na ubishi wa kutokata tamaa

Akupe urahisi wa kuona njia na utatuzi wenye busara kwa kila jambo

Hilo peke ake linatosha kukufanya uishi maisha ya amani, furaha na kuiona Dunia katika jicho Chanya.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Mafanikio Haya Ambukizwi Kwa Ngono

Next Post

Jifunze Kuwa Jeshi La Mtu Mmoja

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.