Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Yaliyopita Si Ndwele Unaweza Kuanza Upya Sasa Na Kubadili Kila Kitu

Umeshawahi kujiuliza kuwa, toka umeanza kufikiria kufanya kitu fulani mpaka sasa kama ungekuwa umefanya kwa vitendo ungekuwa umepiga hatua gani?

Toka ule mwaka ambao ulisema utaanza kufanya kitu fulani, kwa mfano sasa ungefanya kweli! Je ungekuwa umepiga hatua zipi mpaka sasa?

Unaona namna siku zinavyoenda kasi sana? Unaona namna miaka inavyoenda kasi mno!

Anza kuhesabu sasa imepita miaka mingapi toka ulipoanza kufikiria kufanya kitu halafu hukufanya.

Ondoa visingizio vyote na chukulia ungeanza hivyo hivyo kigumu gumu tu, je ungekuwa na hatua gani hadi leo?

Simaanishi ungekuwa na mafanikio makubwa sana, Ila wewe mwenyewe hesabu faida ambazo ungekuwa umepata kama ungeanza wakati ule bila kuacha.

Inawezekana ni biashara fulani ulitaka kufungua ila ukaghairisha

Au ni wazo fulani ulitaka kutekeleza Ila ukapotezea

Lakini pia labda ni akiba ndogo ndogo ulitaka kuanza kuweka Ila ukagairi

Na pengine hata ni mahusiano ulitaka kuanzisha Ila ukaona muda bado

Au tuseme ulitaka kuanza kujenga mwili kwa mazoezi madogo madogo Ila ukaacha tu

Na hata labda ulitaka kuwekeza kwenye kitu fulani kizuri chenye faida Ila tu ukaona uache bila sababu za msingi

Na labda ni Elimu au ujuzi fulani ulitaka kujifunza ila ukagairi tu pasi na sababu za maana.

Sasa hayo yamepita na huna namna yoyote kurudisha siku nyuma,

Ila unaweza kuanza upya sasa hivi kwa namna hio hio uliyonayo kwa sasa

Anza usiogope kabisa, hujachelewa na unaweza kubadili kila kitu miezi michache ijayo

Amua tu kuwa kuanzia muda huu utafanya kitu chako na kamwe hutoacha mpaka uone faida unayotaka.

Leo unaweza kudharau sana Ila kwa namna siku zinavyokimbia utashangaa miaka 2 inaisha ukiwa hujafanya tena!

Usiogope wala kujiona umechelewa anza upya sasa,

Lakini pia usidharau tena kama nyuma, kwani inawezekana usipate wakati mwingine kama huu tena.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Kama Huwezi Kuacha Kinacho Kutesa Basi Pia Hupaswi Kulalamika

Next Post

Huhitaji Maombi Wala Mganga Kuondoa Roho Zinazo Kutesa, Unazo Nguvu Na Uwezo Wewe Mwenyewe

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.