Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Zingatia Alama Zako Za Nyakati Ili Ufanikiwe

Zingatia alama za nyakati kabla hujalaumu ugumu wa mambo na changamoto za maisha

Usilazimishe kufanya kitu kinachokukataa kwa wazi

Sio kila nyakati zinafaa kufanya au kutenda kitu fulani hata kama kina umuhimu mkubwa

Kuna muda unaweza kupitia changamoto na maumivu mengi kwasababu tu haupo kwenye nyakati zako

Kila jambo lina alama zake na muda wake wa kutendeka

Ukiona vikwazo ni vingi zaidi kuliko kawaida basi usilazimishe kufanya kitu hata kama una kihitaji sana maana utaishia kupata majuto na maumivu makali bila mafanikio au hata ukafanikiwa baada ya jasho la meno kutoka wakati lilikuwa jambo dogo tu

Acha upepo mbaya upite kwanza kisha fanya wakati mwingine…

Kuna nyakati mambo huenda yenyewe bila kutumia nguvu kubwa sana

Sio kwamba mafanikio ni marahisi sana au hata magumu sana bali ugumu na urahisi wake upo katika alama sahihi za nyakati unazo pitia,

Hivyo anza kusoma alama zako za nyakati na zihusishe katika mambo unayofanya kila siku

Alama za nyakati Ndio zimebeba siri kubwa sana ya mafanikio bila mateso!

Je unazijua alama zako za nyakati? Kama hapana anza sasa kuzichunguza.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Mbinu Za Kupata wateja

Next Post

Sio Kila Mlango Uliofungwa Pia Umelokiwa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next