Life With Muhasu » You Can Win If You Want

Mafanikio Ni Kama Mimba, Kila Mtu Hukupongeza Akiona Tumbo Kubwa

Yaani mchakato mzima wa upatikanaji wa mimba watu huwa hawaulizi

Mateso yote ya mimba na mahangaiko yake hakuna atakae taka kujua

Shida za mimba, na hata dawa ulizotumia kupata mimba wala watu hawajisumbui kutaka kujua!

Mahudhurio ya kuona madaktari na hata maumivu yote ya kukosa mimba hayupo anae ya hisi zaidi yako

Kuna wale wenye shida na changamoto za uzazi ambao hupitia kebehi na hata matusi mazito kwa walimwengu bado maumivu hubaki kwa mbeba mimba baadae

Hakuna atakae kuwa na wewe na kuhisi mchakato mzima uliofanya kupata mimba

Hakuna atake sema ngoja nikusaidie mateso yako ya mimba

Wala hayupo atae hisi maumivu yote ya kutapika na kushindwa kula kila wakati

Wote husubiri kuona matokeo! Matokeo ya tumbo lilikotuna mbele yako…

Hakika nakuambia hata hayo unayo pitia sasa hivi kuna watu wanaona kama unacheza tu

Wengine wanaona kama umechanganyikiwa tu

Na hata kuna wale hawataki hata kujisumbua kujua unachofanya..

Wote wanangoja siku ufanikiwe wapige makofi ya pongezi!

Kaza moyo safari ya mafanikio haijawahi kuwa rahisi sana wala haipaswi kuwa ngumu sana

Wote ambao huwaoni sasa bado hutowaona ukishindwa!..

Lakini wakisia tu umefanikiwa utashangaa hata uliodhani wamekufa kumbe wapo hai.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Ukitaka Kufanikiwa Bila Kuchoka Fanya Kitu Unacho Kipenda Sana

Next Post

Samaki Mmoja Akioza Muweke Pembeni

Comments 4
Leave a Reply to Mikael Gente Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy makala hii.