
Fanya kitu unacho kipenda zaidi ili kikupe hamasa ya kuendelea
Ni ngumu sana kuendelea kufanya kitu ikiwa huna mapenzi nacho ya dhati
Katika harakati za kutafuta mafanikio jitahidi kuchagua jambo unalo penda zaidi
Hii itakupa wepesi hata pale mambo yanapokuwa magumu sana
Kuna zile nyakati hali inakubana mpaka unatamani kuacha kabisa
Ila ukiwa na mapenzi makubwa na kitu hakika hukufanya upate nguvu upya mara kwa mara
Yaani angalia jambo gani ukilifanya hata kama hutopata faida haraka bado huwezi kulichoka
Chagua kitu ambacho kila ukifikiria kukiacha unaona ni kama umepoteza maana nzima ya kuishi kwako
Fanya jambo ambalo hata kama utakosa shabiki au mteja bado unaweza kujishabikia mwenyewe
Iwe biashara au hata kipaji, ikiwa utakipenda kwa dhati hakika huhitaji mtu mwingine aje kukuambia neno lolote ili upate nguvu
Kitu kikitoka moyoni utajikuta wewe mwenyewe una jishauri na kurekebisha makosa yako hata kama huna mshauri
Hutongoja hamasa ya nje ikupe nguvu ya kuendelea pale unapokwama na kukosa nguvu
Hutotaka kusikia mtu anakuambia acha hakina faida unapoteza muda
Hutoshawishika na tamaa zingine zozote zinazoweza kukutoa nje ya lengo lako
Lakini pia utajikuta unaacha kila kitu kwa ajili ya jambo lako
Utatengeneza mazingira ya kufanikisha hata kama kuna ugumu
Utajikuta bila kutarajia unapata njia na mawazo chanya ya kufanikisha unachotaka
Msukumo wa mapenzi kutoka ndani hutoa nguvu ya ajabu sana kwenye harakati zako
Hutokuwa na kisingizio cha kuamka asubuhi na hata kukesha kwa ajili ya jambo hilo
Na bado utakilinda kwa moyo wote hata kama itatakiwa kutoa kila ulicho nacho kwa ajili ya jambo lako
Na hata kama utafika ukingoni kabisa mwa mawazo na akili ya kufikiria bado uta kuwa king’ang’anizi kwenye hilo jambo
Na mwisho wa siku mafanikio yatakuja kwakuwa tu hukuishia njiani.
Fanya unachopenda sana hakika nacho kitakupenda.
Thank you so much 🙏
Nimeelewa sana 🙏
Karibu sana
Je kwa mtu ambae alikosea kuchagua mwanzoni unamshauri nini?
Kukosea ni kawaida sana Ila ukiona umekosea unapaswa kuanza upya haraka
🙏🙏
Nimeelewa sana 🙏
Andiko zuri. Niko na ushuhuda kwenye hili 😇
Barikiwa sana 🙏
🔥🔥🔥🔥
❤️
“Fanya jambo ambalo hata kama utakosa shabiki, utajishabilia mwenyewe.” ✍️
Hakika be your own fan
Ninapenda sana mambo ya uandishi ila yananishinda, sijui nabidi nifanyeje
Anza kidogo kidogo utazoea
🔥🔥
❤️
😇🙏🙏
🙏
✍️✍️
Asante sana 🙏
Nitarudi kusoma vizuri